Jeshi
la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu 14 kwa tuhuma za makosa mbalimbali.
MAUAJI
Mnamo
tarehe 13.03.2019 majira ya saa 13:30 mchana huko Kitongoji
cha Igadu, Kijiji cha Shuwa, Kata ya Iyunga – Mapinduzi, Tarafa ya Isangati,
Wilaya ya Mbeya Vijijini, Mkoa wa Mbeya. TAMKA
D/O MAMBA @ NGANGALE [28] Mkazi wa Kitongoji cha Masanga “A” aligundua
kuuawa kwa mume wake aitwaye HADSON S/O
HAIWOLE MWANGOKA [45] Mkazi wa Masanga “A” na mtu/watu wasiofahamika.
Marehemu aliondoka
nyumbani tarehe 11.03.2019 saa 05:00
alfajiri kwenda shambani Kitongoji cha Igadu na hakurudi tena, harakati za
kumtafuta zikaanza wakiwa wanamtafuta maeneo ya shambani kwenye korongo ndipo
waliona kiganja cha mkono wa kulia kikiashiria kuna mwili wa marehemu
umefukiwa.
Polisi walifika eneo la
tukio na kukuta kiganja cha mkono korongoni na baada ya kufukua ulikutwa mwili
wa marehemu aliyetambuliwa kuwa ni HADSON
HAIWOLE MWANGOKA huku ukionekana kupigwa kitu kizito usoni. Mwili wa
marehemu umehifadhiwa Hospitali Teule ya Ifisi. Kiini cha tukio ni mgogoro wa
ardhi/shamba la ukoo ambalo alikuwa analima marehemu ambalo linagombewa na wana
ndugu baada ya baba yao kufariki dunia.
Watu nane wamekamatwa
kwa mahojiano kuhusiana na tukio hilo ambao ni 1. PAULO HAIWOLE MWANGOKA [39] mchungaji na mkazi wa Kijiji cha
Sanje 2. FREDRICK MOSES [36] Mkazi
wa Iwindi 3. JOSHUA HAIWOLE [27]
Dereva na mkazi wa Mlima reli 4. MICHAEL
HAIWOLE [18] Mkazi wa Shuwa 5.
ELIZABETH HAIBOLE [62] Mkazi wa Shuwa 6.
JACOB S/O NOAH [51] Mkazi wa Izuo 7.
ELIZA SHEYO [40] Mkazi wa Shua na 8.
ERESIA HAIBOLE [64] Mkazi wa Shuwa. Upelelezi wa shauri hili unaendelea.
TAARIFA
YA KIFO
Mnamo
tarehe 12.03.2019 majira ya saa 13:45 mchana huko Kitongoji
cha Uzunguni, Kijiji cha Idimi, Kata ya Ihango, Tarafa ya Tembela, Wilaya ya
Mbeya Vijijini, Mkoa wa Mbeya. Watoto wawili waliofahamika kwa majina ya 1. CLAVERY MASHAKA [05] na 2. GIFT MASHAKA [03] wote wakazi wa
Idimi walifariki dunia baada ya kusombwa na maji ya mvua yaliyopita kwenye
mfereji uliopo karibu na nyumba yao.
Chanzo cha tukio hili
ni mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha na kutiririsha maji mengi yaliyosababisha
vifo vya watoto hao.
TAARIFA YA KIFO.
Mnamo
tarehe 13.03.2019 majira ya saa 15:00 Alasiri huko maeneo ya
Mtaa wa Lusungo, Kata ya Itende, Tarafa ya Iyunga, Mkoa wa Mbeya, Mtu mmoja
aliyefahamika kwa jina la EZEKIEL BONNY
@ MWAKAPESA, anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 28 – 30 na mkazi wa Itende
alifariki dunia alipokuwa akiogelea kwenye mto Karabwe uliopo mtaa wa Lusungu.
Chanzo cha kifo chake
inasemekana kuwa marehemu alikuwa na tatizo la ugonjwa wa kifafa ambacho
kilimtokea akiwa anaogelea kwenye Mto huo. Mwili wa marehemu umehifadhiwa
Hospitali ya Rufaa Mbeya kwa uchunguzi zaidi wa kitabibu.
Jeshi la Polisi Mkoa wa
Mbeya linatoa tahadhari kufuatia matukio ya kufa maji yanayosababishwa na
uzembe wa kutovaa maboya wakati wanapoingia majini, mtoni au ziwani. Aidha
kufuatia mvua zinazonyesha nawasihi wazazi/walezi kuwa makini na watoto wao kwa
kuweka uangalizi wa kutosha ikiwa ni pamoja na kuwapeleka watoto wadogo Shuleni
na kuwapokea ili kuwalinda dhidi ya madhara ya kutumbukia katika maji au kusombwa
na maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali.
KUPATIKANA NA BHANGI.
Mnamo
tarehe 13.03.2019 majira ya saa 10:45 asubuhi huko katika Kitongoji na Kijiji cha Matondo, Kata
ya Matundasi, Tarafa ya Kiwanja, Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi
wakiwa doria walimkamata JOHN RICHARD [24]
Mkazi wa Kijiji cha Ifyenkenya akiwa na bhangi uzito wa gram 25. Mtuhumiwa ni muuzaji na mtumiaji wa
bhangi.
KUPATIKANA
NA POMBE YA MOSHI NA MTAMBO WA KUPIKIA POMBE YA MOSHI.
Mnamo
tarehe 13.03.2019 majira ya saa 12:00 mchana huko maeneo ya
Sinde “B” Kata ya Sinde, Tarafa ya Iyunga ndani ya Jiji na Mkoa wa Mbeya,
Polisi walimkamata ANATALIA MATUMLA
[44] Mkazi wa Sinde “B” akiwa na pombe ya moshi lita 20 pamoja na mtambo wa kupikia pombe ya moshi. Mtuhumiwa ni muuzaji
na mtumiaji wa pombe hiyo.
KUPATIKANA NA POMBE YA
MOSHI NA MTAMBO WA KUPIKIA POMBE YA MOSHI
Mnamo
tarehe 13.03.2019 majira ya saa 01:30 usiku huko maeneo ya
Sinde, Kata ya Sinde, Tarafa ya Iyunga ndani ya Jiji na Mkoa wa Mbeya, Polisi walimkamata
STELIA ANDALISYE [60] Mkazi wa Sinde
akiwa na pombe ya moshi lita 04
pamoja na mtambo wa kupikia pombe ya moshi. Mtuhumiwa ni muuzaji/mtengenezaji
na mtumiaji wa pombe hiyo.
KUPATIKANA NA POMBE YA
MOSHI
Mnamo
tarehe 13 03.2019 majira ya saa 11:30 asubuhi huko maeneo
ya Kata ya Ruanda, Tarafa ya Iyunga
ndani ya Jiji na Mkoa wa Mbeya, Polisi
walimkamata MAGRET KENYA [45]
Mfanyabiashara na Mkazi wa Mwanjelwa akiwa na Pombe ya moshi lita18. Mtuhumiwa ni muuzaji na
mtumiaji wa pombe hiyo.
KUPATIKANA
NA MTAMBO WA KUPIKIA POMBE YA MOSHI.
Mnamo
tarehe 13.03.2019 majira ya saa 12:00 mchana huko maeneo ya
Ilolo, Kata ya Isanga, Tarafa ya Sisimba ndani ya Jiji na Mkoa wa Mbeya. Polisi
walimkamata DORICE GEORGE [16] Mkazi
wa Ilolo akiwa na mtambo wa kupikia pombe ya moshi. Mtuhumiwa ni mtengenezaji
na muuzaji wa pombe hiyo.
KUPATIKANA NA NYARA ZA
SERIKALI NA POMBE YA MOSHI.
Mnamo
tarehe 13.03.2019 majira ya saa 14:30 mchana huko Kitongoji
cha Mamba, Kijiji na Kata ya Mamba, Tarafa ya Kipembawe, Wilaya ya Chunya, Mkoa
wa Mbeya, Polisi wakiwa doria walimkamata LUCY
ISDORY [47] Mkazi wa Mamba akiwa na vipande15 vya nyama ya Pundamilia vyenye uzito wa kilogram 20 na Pombe Moshi lita 15 akiwa amehifadhi ndani ya nyumba
yake. Upelelezi unaendelea ili kubaini mtandao wa wawindaji haramu na
kuwakamata.
Watuhumiwa wote watafikishwa Mahakamani mara baada
ya upelelezi kukamilika.
Imesainiwa na:
[ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...