Na Emanuel Madafa,Mbeya.
Serikali ya Mkoa wa Mbeya, imesema wataalamu kutoka TANROAD, wameanza zoezi laupembuzi yakinifu wa ujenzi wa Barabara ya Igawa-Tunduma.
Imesema tayari tmu ya wataalamu inaendelea na zoezi hilo na kwamba ujenzi huo wa barabara unatarajia kutumia miezi 14.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila, ameyasema hayo leo, wakati akielezea hatua mbalimbali ambazo serikali inazifanya kwenye utatuzi wa changamoto za miundombinu ya barabara.
“Tayari ujenzi wa barabara kipande cha Igawa hadi Mafinga kimekwisha kamilika, kwahiyo hata hii ambayo imeanza kufanyiwa upembuzi nayo itakamilika kwa wakati “
Hata hivyo kwa mujibu wa Chalamila, amesema pia mchakato wa ujenzi wa barabara ya mchepuko ya Inyara -Mbalizi kwa ajili ya matumizi ya magari makubwa ya mizigo unaendelea.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila,
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...