Anaandika Abdullatif Yunus

Tanzania na Nchi ya Brazil zimeingia makubaliano ya kufufua na kuinua upya Kilimo cha  Pamba Nchini, ili zao hilo liweze kuwa na tija kwa kumnufaisha Mkulima na Taifa kwa ujumla.

Makubaliano hayo baina ya Nchi za Tanzania, Burundi, Kenya na Brazil  yameingiwa mapema Machi 1, 2019 Jijini Mwanza katika Ukumbi wa Belmont Hotel katika Mkutano maalum wa kuinua kilimo cha Pamba "Victoria Cotton Project" ambapo mradi huo utajikita zaidi kuhakikisha wakulima wa zao hili Nchini na Nchi Wadau wanapata pembejeo bora na kwa wakati ,pia uzinduzi wa utafiti unamfikia Mkulima ili aweze kuongeza tija.
 Mh. Innocent Bashungwa Naibu Waziri wa Kilimo, akiwa na baadhi ya wajumbe pamoja na wadau wa zao la Pamba kutoka ndani na nje ya Nchi, wakati walipotembelea moja ya mashamba ya Pamba Jijini Mwanza.
 Pichani ni Balozi wa Brazil Nchini Tanzania Antonio Augusto Martins akizungumza na wajumbe wa Mkutano wa Uzinduzi wa Mradi wa Kuinua Kilimo cha Pamba,(hawapo pichani) uliofanyika Jijini Mwanza, Pembeni ni Naibu Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa.
 Sehemu ya Wajumbe wakiohudhuria Uzinduzi wa Mradi wa Kuinua Kilimo cha Pamba "Victoria Cotton Project" wakifuatilia Mkutano huo Jijini Mwanza.
Pichani ni Naibu Waziri wa Kilimo Nchini, Innocent Bashungwa akichangia katika Mkutano maalumu wa Victoria Cotton Project uliozinduliwa Machi 11, 2019. Jijini Mwanza na kuzishirikisha Nchi za Kenya, Burundi na Brazil.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...