Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle akizungumza wakati akifungua kikao cha wadau kujadili Rasimu ya Muongozo wa Matengenezo ya magari, pikipiki, mitambo, usimikaji na matengenezo ya mifumo ya umeme, elektroniki, viyoyozi, majokofu na kangavuke pamoja na ushauri wa kiufundi kilichohudhuriwa na Wazabuni, wamiliki wa gereji teule, maafisa usafirishaji na wadau kutoka taasisi za Umma na binafsi walioko mkoa wa Dar es Salaam. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Mt. Depot Keko Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle akizungumza na wadau kutoka taasisi za Umma, wazabuni, wamiliki wa gereji teule, maafisa kutoka halmashauri ya mji na maafisa usafirishaji kutoka taasisi za serikali na binafsi walioko mkoa wa Dar es Salaam wakati wa kikao cha kujadili Rasimu ya Muongozo wa Matengenezo ya magari, pikipiki, mitambo, usimikaji na matengenezo ya mifumo ya umeme, elektroniki, viyoyozi, majokofu na kangavuke pamoja na ushauri wa kiufundi kilichofanyika katika ukumbi wa Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau kutoka taasisi za Umma na binafsi, gereji teule, ofisi za halmashauri na wizara mbalimbali kutoka mkoa wa Dar es Salaam wakifuatilia kwa umakini hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa wakati wa kikao cha kujadili Rasimu ya Muongozo wa Matengenezo ya magari, pikipiki, mitambo, usimikaji na matengenezo ya mifumo ya umeme, elektroniki, viyoyozi, majokofu na kangavuke pamoja na ushauri wa kiufundi kilichoandaliwa na Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Uzalishaji na Matengenezo kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Sylvester Simfukwe akitoa ufafanuzi wakati akijibu swali la mmoja wa wadau wakati wa kikao cha kujadili Rasimu ya Muongozo wa Matengenezo ya magari, pikipiki, mitambo, usimikaji na matengenezo ya mifumo ya umeme, elektroniki, viyoyozi, majokofu na kangavuke pamoja na ushauri wa kiufundi kilichoandaliwa na Temesa. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Mt.Depot Keko jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Maafisa usafirishaji, wazabuni, wamiliki wa gereji teule, maafisa tawala na wadau kutoka taasisi mbalimbali za Umma na binafsi zilizopo mkoani humo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...