MBUNGE wa jimbo la Mkuranga Mkoani  Pwani na  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega  ametembelea katika Kitongoji cha  Churwi, Kata ya Tambani na kukaguwa mradi wa kivuko ambapo amefanikiwa kutatua changamoto  ya kivuko hicho chenye historia ya kuuwa watoto wawili.

Akizungumza na wananchi wa eneo hilo, Ulega alisema kuwa ameridhishwa na kitendo cha wananchi kuweza kujichangisha na kuanza ujenzi wa kivuko ili kukabiliana na changamoto zilizokuwa zikiwakabili za kukosa kivuko kwa muda  wa miaka mingi.

Katika hali hiyo  imempelekea Naibu waziri huyo kuchangia mifuko ya saruji 60  na milioni moja na nusu  kuongeza nguvu katika ujenzi wa kivuko hicho.
Aidha  amewataka wananchi hao  kuongeza ushirikiano zaidi katika masuala  ya maendeleo kwani wananchi wanapoanzisha miradi ya maendeleo serikali  ni lazima iweke mkono  wake ili kuongeza nguvu.

"Tushirikiane ili kuokoa maisha ya watoto wetu  pia kivuko hiki  kitasaidia kufungua fursa  mbalimbali za maendeleo kutokana na  uwepo wa uhakika wa njia"Alisema Ulega.Kwa upande  wake diwani wa kata hiyo Ally Mtamirwa amempongeza mbunge  Ulega kwa juhudi zake anazozifanya katika kuhakikisha mkuranga ina kuwa ya kuigwa kwenye maendeleo.

Aliongeza  kuwa bado  wananchi wanaendelea kujitolea katika mambo mbalimbali ya maendeleo ili kuhakikisha wanafanikiwa katika upatikanaji wa huduma za jamii.
Mbunge  wa jimbo la Mkuranga mkoa Pwani,  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akimkabidhi diwani wa kata  ya Tambani, Ally Mtamiwa mifuko 80 ya saruji kwaajili ya ujenzi wa kivuko katika kitongoji cha Churwi kata ya Tambani  wilaya ya Mkuranga.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG)
Mbunge wa jimbo la Mkuranga mkoa Pwani,Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akiweka jiwe la msingi ujenzi zahati ya kijiji cha Tipo  ambapo  alichingia amifuko 50 ya saruji na shilingi milioni moja.
 Mbunge  wa jimbo la Mkuranga mkoa Pwani,  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akiwa ameongoza na niongozi wa chama cha (CCM) wa wilaya hiyo wakigangua mradi wa Zahanati ya kijiji cha Tipo ambapo alichangia mifuko 50 ya saruji na shilingi milioni moja.
Muuguzi wa hospitali ya wilaya ya Mkuranga ,Grace Msemwa akisisitiza jambo katika mkutano uliofanyika katika kijiji cha Tipo wilaya ya hiyo.











Muonekano wa kivuko kinachoendelea kujengwa katika kitongoji cha Churwi kata ya Tambani  wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...