Na Ripota wetu ,Arusha

Timu ya Wataalamu kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), imetembelea Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro NCAA.

Wataalamu hao walitembelea eneo hilo la urithi wa dunia mchanganyiko kutokana na Tanzania kujiunga na kuwa mwanachama wa UNESCO tangu mwaka 1962.

Katika ziara yao timu hiyo ilifanikiwa kutembelea maeneo ya mradi wa ujenzi wa barabara unaotarajiwa kuanza kujengwa hivi karibuni na NCAA kwa kiwango cha tabaka gumu zege ili kurahisha shughuli za utalii, na masuala mengine ndani ya eneo hilo.

Ujio wa timu hiyo umetajwa kuwa ni utaratibu wa kawaida ambapo hutembelea maeneo ya urithi wa dunia kuangalia changamoto za uhifadhi na kutoa ushauri au mapendekezo.

Mkuu wa timu ya wataalamu wa Shirika la Umoja wa Mataifa inaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamduni (UNESCO), Edmound Moukala (katikati), akimsikiliza Kaimu Meneja Idara ya Urithi wa Utamaduni na Mratibu wa UNESCO eneo la NCCA Selestine Ummanuel.

Meneja wa Idara ya Utafiti na Ufuatliaji Mamlaka ya Hifadhi ya gorongoro(NCAA), Julius Kibebe akizungumza kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi NCAA Dk. Fredy Manongi kwenye majumuisho ya ziara ya wataalamu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamduni (UNESCO), waliopo kushoto kwake.

Mkuu wa timu ya wataalamu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamduni (UNESCO), Edmound Moukala akisisitiza jambo kwenye kikao cha majumuisho baada ya kutembelea baadhi ya maeneo ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorogoro.

Pix6. Mwakili wa Baraza la Wafugaji Tarafa ya Ngorongoro akichangia wakati wa majumuisho ya timu ya wataalamu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamduni (UNESCO), waliotembelea maeneo tofauti ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro NCAA. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...