NA REV KADIVA

*20 - 25* = Kama ni kielimu hujafikia malengo yako, sitisha mara moja tafuta kazi/biashara ya kufanya, pigana kufa na kupona ili kama vipi urudi shule kwa pesa yako.

*25 - 30* = Hakikisha uwe na angalau KAZI RASMI kama umeajiriwa au umejiajiri au una shughuli yeyote ya kukuingizia kipato.

*30 - 35* = Uwe na angalau kama sio nyumba basi kiwanja, tena ujitahidi uwe umeoa/umeolewa. Ni vema ukiwa na familia, kwa maana ya kuwa na watoto kama Mungu kakuwezesha.

*35 - 40* = Ni wakati kiwanja kiwe kimejengwa na kama ni tayari basi nenda step nyingine ya kumiliki kama ni Gari au kuongeza nyumba na hakikisha vinaenda sambamba na ongezeko la familia. Hapa inabidi upambane sana kuweka misingi.

*40 - 45* = Ni umri wa masahihisho, kama hukuwahi kununua kiwanja, kama hukujenga basi hapa pambana afe kipa afe beki, ni umri wa masahihisho. Ila kwa wale ambao wameenda vizuri huko nyuma basi hapa watoto wapo kwenye level tofauti za elimu, kwahiyo ni muda wa kuwawekea malengo ya kimasomo watoto wao.

*45 - 50* = Kwa yule ambae hakukosea huko nyuma basi umri huu ni wa kuanza kuwatengenezea mazingira watoto wako, kama ni shughuli zako ni kuanza kuwahusisha, huku wewe ukijiweka pembeni taratibu na kuangalia fursa za umri wako. Lakini kwa wale waliokosea hapa ni kupitia zile hatua za 35 - 40.

*50 - 60* = Ni kujiandaa na maisha mapya ya kustaafu au kujiweka mbali na kazi zinazotumia nguvu au akili nyingi

*60 - 70* = Kula matunda yako huku ukiangalia misingi ya wanao inaendaje.

*70 - 80* = Kula matunda

*80* - nk = Umri wa kusubiria mauti

*Yote kwa yote, maisha yetu yapo mikononi mwa  MUNGU, kumbuka kufanya Ibada wakati wote...*

Inafaa kwa vijana hata kwetu pia ila unaweza kujaribu kujifanya kutoelewa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...