Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika ,tawi la Tanzania (Misa-Tan) Salome Kitomary akizungumza jambo wakati wa Mafunzo kwa watumishi wa Mahakama mkoa wa Kilimanjaro .
Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika ,tawi la Tanzania (Misa-Tan) Salome Kitomary akisikiliza mawazo mbalimbali kutoka kwa washiriki wa mafunzo hayo.
Mkufunzi katika Mafunzo yanayowahusisha watumishi wa Mahakama,Wakili James Marenga akiwasilisha mada katika mafunzo hayo yanayofanyika Hoteli ya Leopard mjini Moshi.
Baadhi ya Washiriki katika mafunzo hayo wakifurahia jambo wakati wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa na wakufunzi.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
VYOMBO vya umma vimetakiwa
kuwasimamia haki ya upatikanaji wa taarifa ikwa ni pamoja na kuwa wakala kwa mwananchi
yoyote atakayehitaji kupata haki isipokuwa kama kuna sheria inayotoa ufafanuzi
wa msingi kwanini zisitolewe.
Hayo yamelezwa na Mkufunzi katika mafunzo kwa watumishi wa
Mahakama yanayofanyika katika Hoteli ya Leopard mjini Moshi,Wakili James
Marenga wakati akiwasilisha mada iliyohusu Muktadha wa Kisheria kwenye haki ya
kupata taarifa.
Alisema haki ya kupata habari inapatikana kwenye mikataba ya kimataifa
ambayo ndimo misingi ya uhuru wa kujielezea imejengeka na kwamba ni tamko la
kimataifa la haki za binadamu la mwaka 1948.
“Ibara ya 19 ya Tamko
hilo inasema kuwa Kila mmoja ana haki
ya uhuru wa kutoa na kueleza maoni yake; haki hii inahusu pia uhuru wa
kutoa maoni yake bila kuingiliwa kati,
na uhuru wa kutafuta na kutoa taarifa na maoni kwa njia yoyote bila kujali
mipaka.” Alisema Marenga.
Alisema katika tamko la Afrika juu ya miiko na kanuni za watumishi wa umma na utawala limeelekeza
kuwa Utumishi wa Umma na Utawala
utahakikisha kuwepo na taarifa na utaratibu wa namna ambavyo utumishi wa umma
unavyotakiwa kutoa huduma.
Marenga alisema utumishi wa umma na utawala wanatakiwa kutoa
taarifa kwa wananchi juu ya mambo yanayowahusu na kama kuna maamuzi juu yao
yametolewa katika misingi gani na kwa sababu gani na kama kuna namna yoyote ya
kukata rufaa juu ya maamuzi hayo.
“ Utumishi wa Umma na Utawala uweke mfumo wa mawasiliano na mchakato
wa kujulisha umma juu ya huduma wanazozitoa ili kuwezesha upatikanaji wa taarifa kwa watumiaji na kupata mrejesho kutoka kwao.
Mapema washiriki wa mafunzo hayo ya siku tatu wameeleza
kupata mwanga zaidi kutokana na mfunzo hayo hasa katika maeneo ya utoaji huduma
kwa wananchi bila kujali hali za wahusika ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kwa
kufuata taratibu zilizoelekezwa kwa mujibu wa Sheria ya upatikanaji taarifa.
“moja ya mambo tunayojifunza ni pamoja na kuacha changamoto
za nyumbani mara baada ya kuingia katika maeneo yetu ya kazi ,na hii husaidia
ufanisi katika kumuhudumia mwananchi ambaye ni mteja wetu “alisema Massawe
mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo.
Mafunzo hayo yanayoendeshwa na Taasisi ya Vyombo vya Habari
Kusini mwa Afrika –Misa Tan kwa kushirikiana na taasisi ya kijerumani ya
Friedrich Ebert Stiftung yamelenga kuwakumbusha watumishi hao wa Mahakam juu
upatikanaji wa taarifa na maadili kwa utumishi wa umma pamoja na utoaji huduma
kwa wateja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...