Na Sultani Kipingo
Wapenzi wawili mjini Cape Town, Afrika ya Kusini, wamefunga ndoa hospitalini siku moja baada ya bwana harusi kushambuliwa na majambazi nyumbani kwake .
Muneer Hercules na Maryam Kallie walifunga pingu za maisha katika hospitali ya Melomed Gatesville Jumapili Machi 10, 2019, huku bwana harusi akiwa kitandani na Bi harusi pembeni yake.
Kwa mujibu wa ukurasa wa Facebook wa Melomed Gatesville, Hercules alikimbizwa hospitalini hapo baada ya kujeruhiwa na majambazi nyumbani kwake Jumamosi Machi 9.
"Asubuhi hii Muneer Hercules na Maryam Kallies wamefanya Nikkah mbele ya watu wa familia zao hapa  Melomed Gatesville Hospital. Muneer alishambuliwa usiku wa kuammia leo na kukimbizwa hospitali.” Ameandika  Melomed.
Hata hivyo, shambulizi hilo halikuzuia wapenzi hao kuoana kwa taratibu za Kiislamu hapo hospitali, na mapicha kibao yaliyo kwenye ukurasa wa Melomed yanaweza kukufanya utokwe na chozi.
Maryam alikuwa amevaa shela lake nzuri nyeupe huku mkononi kashikilia maua wakati akiingia hospitalini hapo, wakati mumewe mtarajiwa akiwa anasubiri kwa hamu kitandani huku akipigana na maumivu, bila shaka akimshukuru Mola kwa kumjaalia mwenza atayeishi naye kwa shida na raha. 
 Muneer Hercules na Maryam Kallie wakikumbatiana baada ya kufunga za maisha katika hospitali ya Melomed Gatesville Jumapili Machi 10, 2019, 
Muneer Hercules na Maryam Kallie walifunga pingu za maisha katika hospitali ya Melomed Gatesville Jumapili Machi 10, 2019, 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...