WIZARA ya afya kwa kushilikiana na Mradi wa USAID Tulonge
Afya fhi 360 wametoa mafunzo kwa wanahabari jijini Mwanza
juu ya utoaji habari wakati wa maandalizi ya uzinduzi wa
Majukwaa mawili ya mawasiliano ya afya kwa watu wazima
litakaloitwa “NAWEZA” na kwa vijana “SITETELEKI” ili
kufikisha elimu sahihi itakayoijengea jamii ya Watanzania
uwezo na kubadilisha mitizamo na tabia zao za kiafya na kuleta
matokeo chanya.
Mafunzo hayo yalifanyika jijini Mwanza mwishoni mwa wiki
katika Hotel ya Gold Crest ambapo yalipata mwitikio mkubwa
na ulewa mzuri kwa wanahabari waishio jijini Mwanza.
Mafunzo hayo yaliendeshwa na wataalamu mambo ya Afya
kutoka Wizara ya Afya na USAID Tulonge Afya fhi 360.
NAWEZA ni jukwaa litakalolenga kuwafikia wananchi tofauti
tofauti itachangia kuboresha afya na ustawi wa Watanania
wengi, itakuwa ikibadilika badilika ili kukidhi mahitaji ya
maeneo mengine ya kiafya muhimu kwa walengwa hao ama
makundi mengine hususani watu wazima.
SITETELEKI ni jukwaa litakalolenga zaidi kuwafikia Vijana
wenye umri kati ya 15 – 24, wanaokabiliwa na changamoto
nyingi za malengo ya maisha.
Mratibu
wa Afya ya Uzazi Wizara ya Afya, Martha Shakinyau(kushoto) akizungumza
na Wanahabari jijini Mwanza wakati wa mafunzo ya awali ya namna ya
utoaji taarifa kwa jamii juu ya amajukwaa mawili yanayotarajiwa
kuzinduliwa hivi karibuni ya NAWEZA NA SITETELEKI.Kulia ni baadhi ya
Wanahabari wa jijini Mwanza wakimsikiliza Mratibu huyo.Mafunzo hayo
yalifanyika katika Hotel ya Gold Crest jijini Mwanza.
Mkurugenzi
wa Mawasiliano wa USAID Tulonge Afya, Prisca Rwezahura(kushoto)
akizungumza na Wanahabari jijini Mwanza wakati wa mafunzo ya awali ya
namna ya utoaji taarifa kwa jamii juu ya majukwaa mawili yanayotarajiwa
kuzinduliwa hivi karibuni ya NAWEZA NA SITETELEKI.Kulia ni baadhi ya
Wanahabari wa jijini Mwanza wakimsikiliza Mratibu huyo.Mafunzo hayo
yalifanyika katika Hotel ya Gold Crest jijini Mwanza.
Wanahabari
wa Jijini Mwanza wakifuatili kwa makini mafunzo ya awali ya namna ya
utoaji taarifa kwa jamii juu ya majukwaa mawili yanayotarajiwa
kuzinduliwa hivi karibuni ya NAWEZA NA SITETELEKI..Mafunzo hayo
yalifanyika katika Hotel ya Gold Crest jijini Mwanza mwishoni mwa wiki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...