WIZARA ya Afya kwa kushirikiana na Mradi wa USAID
Tulonge Afya fhi 360 wametoa mafunzo kwa wanahabari
mkoani Tabora juu ya utoaji habari baada ya uzinduzi wa
majukwaa mawili ya mawasiliano ya afya kwa watu
wazima ‘NAWEZA’ na vijana ‘SITETELEKI’ yanayotarajiwa
kuzinduliwa hivi karibuni.
Majukwaa hayo yanalenga kufikisha elimu sahihi itakayoijengea
jamii ya Watanzania uwezo ili kubadilisha mitizamo na tabia zao
za kiafya na kuleta matokeo chanya.
Mafunzo hayo yamendeshwa na wataalamu wa masuala ya afya
kutoka Wizara ya Afya na USAID Tulonge Afya fhi 360
yalifanyika leo katika Hotel ya Rastalemi mjini Tabora na
kupata mwitikio mkubwa na uelewa mzuri kwa wanahabari wa
mkoani humu yakiwa ni maandalizi ya uzinduzi wa majukwaa
hayo ya NAWEZA na SITETEREKI mkoani humo.
Mtaalamu wa mambo ya Afya kutoka Wizara ya Afya, Oscar
Kapera alisema NAWEZA ni jukwaa linalolenga kuwafikia
wananchi tofauti tofauti na itachangia kuboresha afya na ustawi
wa Watanzania wengi, itakuwa ikibadilika badilika ili kukidhi
mahitaji ya maeneo mengine ya kiafya muhimu kwa walengwa
hao ama makundi mengine hususani watu wazima.
Meneja
wa Fhi Tulonge Afya Kanda Kaskazini na Kati, Dkt. Benedict Kafumu
akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mafunzo ya awali ya namna
ya utoaji taarifa kwa jamii juu ya majukwaa mawili yanayotarajiwa
kuzinduliwa hivi karibuni ya NAWEZA NA ITETELEKI. Mafunzo hayo
yamefanyika leo katika Hoteli ya Ristalemi mjini Tabora.
Afisa
wa Afya kutoka Wizara ya Afya, Oscar Kapera akizungumza na waandishi wa
habari wakati wa mafunzo ya awali ya namna ya utoaji taarifa kwa jamii
juu ya majukwaa mawili yanayotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni ya
NAWEZA NA SITETELEKI.Mafunzo hayo yalifanyika leo katika Hoteli ya
Ristalemi mjini Tabora.
Mtaalamu Mkongwe wa Ushauri wa mambo ya Afya kutoka Fhi Tulonge
Afya, John Bosco Basso akizungumza jambo wakati wa mafunzo ya awali
ya namna ya utoaji taarifa kwa jamii juu ya majukwaa mawili
yanayotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni ya NAWEZA NA SITETELEKI.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...