Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Salama Aboud Talib (katikati) akikata keki kuashiria uzinduzi rasmi wa matumizi ya mtandao wa Simu ya TTCL kulipia huduma za maji kupitia T-Pesa. Tukio hilo limefanyika sambamba na Maadhimisho ya kilele cha Wiki ya Maji, yenye kauli mbiu 'Hakuna Atakae Achwa'. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Waziri Kindamba.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Waziri Kindamba (kulia) akimkabidhi zawadi ya simu ya mkononi Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Salama Aboud Talib (kushoto) kwenye hafla ya uzinduzi rasmi wa matumizi ya mtandao wa Simu ya TTCL kulipia huduma za maji Zanzibar kupitia T-Pesa.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Waziri Kindamba (kulia) akimwelekeza Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Salama Aboud Talib (kushoto) namna ya kufanya malipo ya bili ya maji Zanzibar kupitia T-Pesa.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Waziri Kindamba (kulia) akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi rasmi wa matumizi ya mtandao wa Simu ya TTCL kulipia huduma za maji kupitia T-Pesa.
Mkurugenzi wa Biashara na Huduma kwa Wateja wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA), Kazija Mussa Msheba (kushoto) akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi rasmi wa matumizi ya mtandao wa Simu ya TTCL kulipia huduma za ZAWA kupitia T-Pesa. Kwa makubaliano hayo sasa wateja wa ZAWA watakuwa wakilipa bili zao kupitia mtandao wa T-Pesa.
Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Salama Aboud Talib (katikati) akionesha simu ya mkononi aliyokabidhiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Waziri Kindamba (kuliye aliyeshika kipaza sauti) kama zawadi.
Baadhi ya washiriki kwenye hafla ya uzinduzi rasmi wa matumizi ya mtandao wa Simu ya TTCL kulipia huduma za Mamlaka ya Maji Zanzibar kupitia T-Pesa wakifuatilia matukio anuai. Kwa sasa wateja wa ZAWA watakuwa wakilipa bili zao kupitia T-PESA.
Baadhi ya wafanyakazi wa TTCL (kushoto) wakiwaelekeza washiriki namna ya kulipia huduma za ZAWA kupitia T-Pesa.
Wateja wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) wakipata maelekezo namna ya kulipia bili kwa T-PESA.
Picha ya pamoja na meza kuu mara baada ya hafla hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...