Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii.
Wakazi wawili wa Chanika jijini Dar es Salaam, Abdallah Hamis (30) na Adam Kawambwa(35)  wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na tuhuma za kukutwa na meno ya tembo yenye thamani ya zaidi Sh  bil.moja na utakatishaji.

Akisoma hati ya mashtaka, mbele ya Hakimu Mkazi, Augustine Rwizile Wakili wa serikali Candid Nasua amedai, washtakiwa wametenda makosa yao Februari 11.2019 huko Chanika kwa Zoo katika Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam. Imedaiwa siku ya tukio washtakiwa walikutwa na vipande 47 vya meno ya tembo vyenye thamani ya USD 465,000 ambayo ni sawa na Sh. 1,081,375,500 mali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania bila ya kuwa na kibali kutoka kwa mkurugenzi wa wanyama pori.

Katika shtaka la pili imedaiwa Siku na mahali hapo, washtakiwa hao walikutwa na vipande hivyo vya meno ya Tembo huku huku wakijua kuwa wamepata vipande hivyo kutokana na kutenda kosa la ujangili. Hata hivyo, washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo  kwa sababu Mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi ambazo kwa kawaida zinasikilizwa Mahakama Kuu au mpaka pale itakapopata kibali kutoka kwa DPP.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka, upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika na imeahirishwa hadi Machi 25,2019 itakapokuja kwa ajili ya kutajwa.
 Watumiwa Abdala Hamis na Adam Kawabwa wakiingia mahamani kisutu kwa kosa la kukutwa na meno ya Tembo yenye thamani ya thamani ya USD 465,000 thamani ya Sh. 1,081,375,500  na utakatishaji.
Washtakiwa Abdallah Hamis (30) na Adam Kawambwa(35) wakitoka katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo wanakabiliwa na tuhuma za kukutwa na meno ya tembo yenye thamani ya USD 465,000 thamani ya Sh. 1,081,375,500  na utakatishaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...