Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia), akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, wakati wajumbe hao walipotembelea eneo litakalojengwa Jengo la Makao Makuu ya Uhamiaji, Jijini Dodoma, leo. Ujenzi wa jengo hilo ambao tayari umenza, unatarajiwa kukamilika baada ya miezi 16. Katikati aliyevaa kofia ni Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Victor Mwambalaswa. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.   

Katibu wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Ramadhan Abdallah, akitoa taarifa ya Kamati hiyo, katika kikao chao na Watendaji Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kilichofanyika katika ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dodoma, leo. Kushoto meza kuu ni Waziri wa Wizara hiyo, Kangi Lugola. Katikati ni Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Victor Mwambalaswa. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.  
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto), na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu (katikati), wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Idara ya Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala, alipokuwa anawafafanulia jambo katika eneo la ujenzi wa Makao Makuu ya Idara hiyo, jijini Dodoma, leo.  Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.   

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia), akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, Jijini Dodoma, leo. Mara baada ya kikao hicho, wajumbe hao walitembelea eneo litakalojengwa Jengo la Makao Makuu ya Uhamiaji, Jijini Dodoma. Ujenzi wa jengo hilo ambao tayari umenza, unatarajiwa kukamilika baada ya miezi 16. Kulia ni Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Victor Mwambalaswa. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...