Hitimisho la Wiki ya Maji Duniani, Mamlaka ya MajiSafi na MajiTaka (DAWASA) wamewapa furaha wakazi wa Saranga na maeneo jirani kwa kuwapatia maji safi na salama. Akizungua wakati wa kuzindua mradi wa kuwasambazia maji wakazi wa Saranga Mkuu wa Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam Kisare Makori amesema kuwa amefurahishwa jinsi DAWASA walivyoweza kuwapa furaha wakazi hao wa Saranga kwa kuwapatia maji ambayo watakuwa wakiyapata masaa 24. Mkuu wa Wilaya ya Ubungo jijini Dar es S  alaam Kisare Makori (kushoto) akimpongeza Kaimu Mkurugenzi wa miradi DAWASA Lydia Ndibalema kwa kuweza kufanikisha uwekaji wa bomba eneo la Saranga jijini Dar es Salaam. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
 Mkuu wa Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam Kisare Makori (kushoto) akimpongeza Kaimu Mkurugenzi wa miradi DAWASA Lydia Ndibalema kwa kuweza kufanikisha uwekaji wa bomba eneo la Saranga. Wengine wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam Kisare Makori (kushoto) akizungumza na wakazi wa Saranga (picha ya chini) Kaimu Mkurugenzi wa miradi DAWASA Lydia Ndibalema akizungumza na wakazi wa Saranga jijini Dar es Salaam kuwaelezea jinsi walivyoweza kufanikisha kufikisha mradi huo.
Meneja wa DAWASA- Kimara jijini Dar es Salaam Paschal Fumbuka akielezea jinsi mradi ulivyoweza kukamilika wakati wa hitimisho la wiki ya Maji Duniani iliyoanza Machi 16-22, 2019.
Diwani wa kata ya Saranga Mhe. Haruni Mdoe akizungumza na wakazi wa Kimara Tembeni kata ya Saranga jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam Kisare Makori (wa tatu kutoka kushoto) akikata utepe na Diwani wa kata ya Saranga Mhe. Haruni Mdoe kuzindua huduma hiyo.
Tukio Lingine alilolifanya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Makori ni kuzindua eneo la Bomba la Kwanza lililowekwa kwa mkazi mmoja wa Saranga ili kuonyesha ishara ya usambazaji wa maji kwa wakazi hao.
Wakazi wa Saranga wakijiandikisha mbele ya wenyekiti wa Serikali za mtaa ili waweze kupatiwa maji na DAWASA.
Meneja wa huduma kwa wateja wa DAWASA Doreen Kiwango akiangalia zoezi la uandikishaji wateja wapya wakazi wa Saranga linavyoendelea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...