Na Woinde Shizza globu ya jamii

MTU mmoja alietambulika kwa jina la Lazaro Keorori (53) mkazi mtaa Wa Simanjiro Kata ya Sombetini amefariki dunia Mara baada ya kujichinja chinja na kisu kikali.

Akizungumza na waandishi Wa habari kamanda Wa polisi mkoa Wa Arusha Jonathan Shana alisema kuwa tukio hilo limetokea aprili 15 majira Saa moja asubui . 

Alibanisha kuwa uchunguzi ulifanywa na jeshi la polisi umebaini kuwa marehemu amechukuwa uwamuzi huo kutokana na mgogoro Wa kifamilia uliokuwepo kati yake nawake zake wawili .

"Marehemu alikuwa na msongo Wa mawazo uliompelekea yeye kuamua kuchukuwa uamuzi Wa kujiuwa ,na kwamaelezo ya watu waliohojiwa walisema aliingia ndani usiku akachukuwa kisu kidogo chenye makali akaanza kujichinja sasa ,pamoja alikuwa chumbani watu waligundua Saa ile ambapo roho ilikuwa inataka kutoka akawa anapiga kelele ndio watu wakamjua ila haikuwezekana kumuokoa roho take" alisema kamanda

Aidha aliwaasa wananchi haswa wanafamilia wakiwemo wanaume kutochukuwa maamuzi ya haraka haraka na kuwasihi iwapo wakipata msongo Wa mawazo ni vizuri wakaenda kupewa ushauri katika nyumba za ibada au katika familia na sio kujichukulia sheria mkononi.

Wakati huo huo jeshi la polisi linawashikilia watu Tisa kwa makosa ya kuwatapeli watu Aridhi.Kamanda Wa polisi amesema kuwa sasa ivi mkoa Wa Arusha umegubikwa na wimbi la matapeli ambapo wanajidai wao ni maafisa ardhi ,huku wengine wakijifanya ni matajiri wanunuaji huku wengine wakijidai ni wenye mashamba .

Aisha alibainisha kuwa jeshi la polisi limefanya operation na kuwakamata watu Tisa ambapo kati yao wawili ni wafanyakazi Wa halmashauri ya jiji la Arusha ,huku wawili wakiwa ni wafanyakazi Wa ofisi ya Aridhi Kanda ya kaskazini na wengine sita waliobaki ni wananchi Wa kawaida.

Kamanda alisema kuwa watu hao watafikishwa mahakamani pindi tu upelelezi utakapo kamilika ,pia alitoa wito kwa wananchi kufuata sheria na kufanya uchunguzi kabla ya kununua au kuuza nyumba au kiwanja.

Picha kamanda Wa polisi mkoa Wa Arusha Jonathan Shana akionyesha waandishi Wa habari kisu ambacho marehemu Lazaro Keurori alitumia kuji chinjia chinjia .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...