DICKSON Archibold Maro (53) amekutwa amefariki dunia ndani ya gari IT, aina ya noah yenye namba za cheses 603026045 baada ya kuugua ghafla. 

Kamanda wa polisi mkoani Pwani, ACP Wankyo Nyigesa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, karibu na kituo cha mafuta cha state oil, huko Mdaula, Bwilingu Chalinze mkoani Pwani. 

Alisema gari hiyo ilikuwa ikitokea Dar es salaam kuelekea Tunduma mkoa wa Songwe. "Baada ya kufika kituo cha mafuta cha state oil, marehemu aliugua ghafla akiwa amepaki gari eneo hilo "alifafanua Wankyo. 

Wankyo alielezea, wahudumu wa kituo hicho walitoa taarifa kwa askari polisi ambao walifika mara moja na kukuta marehemu akiwa na hali mbaya. 

Jitihada za kumuwahisha marehemu kituo cha afya Chalinze zilifanyika lakini baada ya kufikishwa kituoni hapo aligundulika amekwishafariki.

Hata hivyo, Kamanda huyo alisema kwamba, marehemu Dickson alipopekuliwa alikutwa na shilingi 285, 000 pamoja ,dola 400, simu mbili aina ya itel , tecno na karibu na gia kulikutwa chupa mbili za maji na chupa ya juice zilizonywewa. 

Wankyo alisema, utaratibu unafanyika kwa kushirikiana na clearance agency wanaohusika na upatikanaji wa bidhaa kutoka nchi moja kwenda nyingine ili liweze kuondolewa kituo cha polisi Chalinze ambapo limehifadhiwa. 

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospital ya rufaa ya Tumbi kwa uchunguzi wa daktari na ndugu wa marehemu wamejitokeza ili baada ya uchunguzi wakabidhiwe mwili huo kwaajili ya mazishi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...