katibu mkuu wizara ya elimu sayansi na teknolojia Dokta Leonard Akwilapo amesema hali ya uzalishaji wa chakula nchini inaelezwa kuwa ndogo,ambapo takwimu za uzalishaji za mwaka 2015 zinaonesha kuwa ni asilimia tatu nukta tatu kwa mujibu wa mpango wa Taifa ya maendeleo ya awamu ya pili 2016/ 2017, 2020/ 2021 ambapo mpango wa serikali unatajwa kupandisha kiwango hicho kufikia asilimia nne nukta sifuri ifikapo kabla ya mwaka 2025…

Katika kuhakikisha malengo hayo yanafikiwa,Katibu mkuu wizara ya elimu sayansi na teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo anatumia kumbukizi ya miaka kumi na sita ya kifo cha hayati Edward Moringe Sokoine kukiagiza chuo kikuu cha Sokoine (SUA ) kuhakikisha kinatumia wataalamu wake katika kufanikisha dhana hiyo.

“kwa pamoja tunakazi kubwa ya kufanya ili kufikia lengo hili kilimo chetu kinapaswa kukuzwa na kuwa cha kisasa Zaidi” alisema dkt akwilapo. Pia katibu mkuu amehaidi kutoa million 750 kutoka mradi wa kukuza ujuzi na stadi za kazi kwa ajili ya kuboresha kalakala ya idara uhandisi kilimo katika chuo hicho cha kilimo SUA..

Kwa upande wake makamu mkuu wa chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Profesa Raphael Chibunda amesema chuo kimeaandaa mdahalo kwa kuwakutanisha wanasanyansi na watu ambao wamefanya kazi pamoja na Sokoine ili kupata kwa kiina yale aliyofanya Marehemu huyo ambapo mada kuu ni Uzalishaji wa kilimo na Viwanda na Maendeleo ya Tanzania mabo ya kujifunza kutoka kwa sokoine na na siku zijazo..

“Tumewaalika wazee waliofanya kazi na hayati sokoine enzi za uhai wake na wametukubalia ambao watatupatia uzoefu wa namna ya utendaji wake enzi za uhai wake jambo litakalokuwa na tija kwetu” alisema Prof chibunda.. mwakilishi wa familia ya aliyekuwa waziri mkuu wa serikali ya awamu ya kwanza hayati Edward Moringe Sokoine Bw. Ole Edward amesema kama familia wameanda wakfu ili kuendelea kuyaenzi yale aliyofanya marehemu Sokoine…

Hayati Edward Moringe Sokoine alifariki aprili 12 mwaka 1984 katika eneo la Wami sokoine wilayani Mvomero akitokae Bungeni katika majukumu ya kikazi na wiki ya kumbukikizi hiyo imeanza aprili 9 mwaka huu na inatarajiwa kufikia kilele aprili 12 mwaka huu na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Raisi mama samia Suluhu Hassani.
 Katibu mkuu wizara ya elimu sayansi na teknolojia Dokta Leonard Akwilapo kulia akiwa na makamu mkuu wa chuo kikuu cha Sokoine cha  Kilimo SUA Profesa  Raphael Chibunda wakitazama moja ya njia rafiki ya kkilimo ch

 Katibu mkuu wizara ya elimu sayansi na teknolojia Dokta Leonard Akwilapo, wa pili kutoka kushoto akiambatana na katibu tawala mkoa wa morogoro cliford tandari katika ukaguzi wa miradi mbalimbali ya kilimo chuo cha Sokoine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...