Mwenyekiti wa Bodi ya Tatu ya Maji ya Taifa Prof.Hudson Hamis Ngotagu (mwenye miwani) pamoja na wajumbe wa bodi, na baadhi ya watendaji wa Wizara ya Maji wakikagua mtiririko wa maji katika kituo cha upimaji cha Mzinga Konga, mkoani Morogoro. Mtiririko wa maji kuelekea katika bwawa la Mindu linalotegemewa kama chanzo cha maji mjini Morogoro umebainika kupungua kwa sababu ya matumizi yasiyofaa ya maji na shughuli nyingine za kibinadamu. 
Hali halisi ya mtiririko wa maji katika kituo cha Mzinga-Konga, vipimo vikionyesha kiwango cha maji yalivyopungua. 
1 Taswira ya hali ya maji katika bwawa la Mindu ambalo ni chanzo cha maji katika mji wa Morogoro. Kiwango cha maji kinachoonekana kinatakiwa kuongezeka kwa mujibu wa wataalam kwa kulinda mtiririko wa maji. Mito inayotiririsha maji katika bwawa la Mindu maji yake yamechepushwa au kubadilishwa mwelekeo kutokana na shughuli za kilimo ikiwamo mto Mlali na mto Mgera. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...