-Mwenyekiti Taifa wa Chama cha lliance For Democratic Change(Diara ya Mabadiliko-ADC)Hamad Rashid akisisitiza jambo alipokua akitoa hotuba ya Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama hicho uliofanyika Hoteli ya Madinatul Bahri Chukwani Zanzibar.
Mwenyekiti Taifa wa Chama cha lliance For Democratic Change(Diara ya Mabadiliko-ADC)Hamad Rashid akitoa hotuba ya Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama hicho uliofanyika Hoteli ya Madinatul Bahri Chukwani Zanzibar.
Baadhi ya Wageni Waalikwa wavyama mbalimbali waliohudhuria katika Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha ADC uliofanyika Hoteli ya Madinatul Bahri Chukwani Zanzibar.
Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Alliance For Democratic Change(Diara ya Mabadiliko-ADC)waliohudhuria katika Mkutano huo uliofanyika Hoteli ya Madinatul Bahri Chukwani Zanzibar.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance For Democratic Change (Dira ya Mabadiliko-ADC)Queen Althbat Sendiga akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Chama hicho uliofanyika Hoteli ya Madinatul Bahri Chukwani Zanzibar.
Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance For Democratic Change(Diara ya Mabadiliko-ADC)Doyo Hassan Doyo akitoa hotuba ya makaribisho kwa Mgeni Rasmi katika Mkutano Mkuu wa Chama hicho uliofanyika Hoteli ya Madinatul Bahri Chukwani Zanzibar.
….

NA Rahma Khamis Maelezo Zanzibar

Mwenyekiti wa Chama cha ADC Taifa Hamad Rashid Mohammed amewataka wanachama wa chama hicho kufuata ilani yao kwa vitendo ili kupambana na vitendo viovu ikiwemo rushwa na wizi uliyomo katika jamii.

Ameyasema hayo huko Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar katika Ukumbi wa Madinat Al Bahri wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama hicho.

Amesema msingi wa Mkutano huo unatokana na matakwa ya katiba ya ADC ambao ndio dira ya maendeleo ya wananchi katika kufikia malengo ya kuchagua viongozi ambao wanaweza na hatimae kushika dola.

Aidha amesema kuwa mkutano huo utawezesha kutambua changamoto zinazowakabili wanachama na kutoa mafunzo ya mara kwa mara ili kutatua changamoto hizo zinazowakabili. Mwenyekiti huyo amefahamisha kuwa umakini wa uongozi wa chama ndio msingi unaohitajika kwani ndio unaoleta maendeleo na kuweza kupata wanachama wapya ambao ndio watakaofikisha chama hicho kule wanakokuhitaji.

Akizungumzia suala la kisiasa amesema kuwa Duniani kote wanazingati a hali ya usalama na amani hivyo anazipongeza Serikali zote mbili kwa kudumisha amani na utulivu uliopo Nchini. Pia amefafanua kuwa ADC ina uwezo wa kusimamia hali ya usalama na amani na ndio mana imefanikiwa hadi leo kufikia Mkutano Mkuu wa chama Taifa na kuchagua Viongozi watakaoweza kusimamia na kuleta maendeleo.

Amesema kuwa suala la Bima ya Afya lazima lifanyiwe kazi ili kuwapunguzia wananchi gharama za matibabu sambamba na kufanikiSha afya bora kwa kila mwananchi. Hata hivyo Hamad Rashid anaunga mkono Serikali suala la elimu bure hadi kufikia chuo kikuu lakini kwa upande wao wamsema kuwa ni hatua kawa hatua hadi kufikia lengo hilo.

Nae Naibu Katibu Mkuu wa chama ADC Queen Alithbert Sendiga amesema kuwa katika uchaguzi mkuu ujao 2020 anatarajia kugombea nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia ADC ili kuweza kuwainua wanawake kimaendeleo.

Aidha amefahamishakuwa wanawake wengi ndio wanaokuwa mbele katika kushiriki mambo mbalimbali laikini wanarudi nyuma kutokana na changamoto zinazowakabili ikiwemo mila na taratibu zinazowazuwia kugombea nafasi hizo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...