Nteghenjwa Hosseah, Mlowa Chamwino
Ni wiki moja sasa tangu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  Selemani Jafo (Mb) kutembelea eneo la ujenzi wa hospital ya Wilaya ya Chamwino inayojengwa katika Kata ya Mlowo ambapo alikuta kusuasua kwa ujenzi wa hospital hiyo ilihali fedha zilishapokelewa zaidi ya miezi mitano iliyopita: Hali hiyo ilimpelekea kutoa agizo la kuendelea kwa ujenzi huo haraka

Hivi leo Waziri Jafp amerejea tena katika eneo la ujenzi wa hospital hiyo na kiushuhudia ujenzi ukiwa unaendelea kwa kasi na majengo zaidi ya matatu yakiwa yameshaanza kupanda na mengine yakiwa yanakamilishwa kwenye hatua ya jamvi.

Mafundi wa kutosha wakiwa wanaendelea na shughuli za ujenzi katika eneo la Mlowo huku Menejiment ya Chamwino nayo ikitoa muongozo wa nini cha kufanya sambamba na Kamati ya Ulinzi na Usalama ikiwa inahakiki kuwa kitu kitu kinaenda kama kilivyopangwa ni miongoni mwa vitu vilivyomfanya Waziri Jafo kurejesha Imani na Halmashauri hii kuwa wamejipanga kukamilisha jengo leo ndani ya muda kama alivyoagiza.

Akizungumza katika ziara hiyo Jafo amesema amefurahi kuona ujenzi wa Hospital ya Wilaya umefikia katika hatua nzuri na kuwataka watendaji wa Chamiwno kuendelea na kasi hiyo  ili Hospital hiyo iweze kumailika mapema na iwe yenye ubora wa hali ya juu.
“Leo naweza kuwapongeza mmefanya kazi kubwa ndani ya wiki moja niliyowapa sasa nataka ikifika tarehe 12 Mei majengo ya Hospital hii yawe yamefikia hatua siyo chini ya Lenta kwa majengo yote saba tayari kwa kuezeka na kuanzia tarehe 25 Mei majengo yote yawe yamepauliwa kwa Hospitali” alisisitiza Jafo.

Wakati huo huo Jafo ameugiza Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kuanza kupanga Wilaya hiyo kwa mujibu wa sheria za mipango miji ili uweze kuendana na hadhi ya Makao Makuu ya Nchi.
“Chamwino iko karibu sana na Jiji la Dodoma na Jiji hivi sasa wanaenda kwa kasi sana katika upangaji wa maeneo, wanapima viwanja wanauza na wanaongeza mapato yao lakini sioni izo jitihada katika Wilayah ii na nyie ndipo sehemu ambapo Ikulu imejengwa mnatakiwa mjiongeze muanze kupima maeneo na kuuza ili muongeze na mapato ya Halmashauri yenu” alisema Jafo.

Aliongeza kuwa katika eneo hili la Mlowo ambapo hospital inajengwa mngenza kufanya mikutano na wananchi ili mkubalien utaratibu sahihi utakaotumika katika kupima maeneo ya wakazi lakini pia kutafuta maeneo ambayo Halmashauri inaweza kuyanunua, kuyapima na kuyauza kwa wahitaji; Mhakikishe mmetnga maeneo ya huduma za kijamii, makazi, biashara na uwekezaji hii itawasisia sana katika kuongeza mapato.

Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino ilipata shilingi Bil 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospital ya Wilaya mapema mwezi Oktoba – Novemba, 2018 na mpaka sasa ujenzi huo unaendelea vizuri.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  Selemani Jafo akiwasili katika eneo la Mlowo inapojengwa Hospital ya Wilaya ya Chamwino kwa ajili ya ukaguzi wa majengo hayo.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo akikagua ujenzi wa Hospital ya Wilaya ya Chamwino wakati wa ziara yake Wilayani humo.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo kitoa amelekezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Vumilia Boga pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ndg. Athumani Masasi wakati wa ziara yake kukagua ujenzi wa Hospital ya Wilaya katika eneo la Mlowo.
Muonekano wa jengo mojawapo katika ya majengo saba yanayojengwa kwa ajili ya Hospital ya Wilaya ya Chamwino.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...