MKUU wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiongea na wanafunzi na viongozi wa chuo kikuu cha Iringa waliokuwa kwenye mkesha wa kuabudu na kuomba na kuwataka waamini wote kujiandaa kabla hawajaanza kusali ili kuweza kuyafikisha maombi yao vilivyo kwa mwenyezi mungu. 
MKUU wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiwa kwenye picha ya pamoja na moja ya kwaya iliyota burudani siku hiyo ya mkesha wa kuabudu na kuomba
Baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuku cha Iringa wakiwa kwenye mkesha huo.


NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

MKUU wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amewataka waamini wote kujiandaa kabla hawajaanza kusali ili kuweza kuyafikisha maombi yao vilivyo kwa mwenyezi mungu.

Akizunguza wakatika wa mkesha na kuambudu kwa wanafunzi wa chu kikuu cha Iringa mkoani Iringa Kasesela alisema kuwa wa kila jambo ambalo unatarajia kulifanya ni lazima ujiandae kwanza.

“Mimi katika maisha yangu kabla sijafanya jambo huwa natafuta muda wa kulifikiria jambo hilo ndio nalifanyia kazi ndio maana mara nyingi nimekuwa na maamuzi sahihi katika kufanya kazi zangu kila wakati” alisema Kasesela

Kasesela aliwataka wanafunzi hao kufanya maombi ya kukiombea chuo hicho ili kuendelea kuwa chuo bora hapa nchini na nje ya nchi na kuendelea kuutangaza mkoa wa Iringa kwa kuwa jina la chuo hicho limebeba jina la mkoa wa Iringa.

“Chuo hiki kilitaka kufungwa kwa ajili ya mambo ambayo hayana miguu wa kichwa hivyo naowaomba mkiombee chuo hiki ili kisije kikafungwa au kufikiriwa kufungwa tena maana kimekuwa kikitoa elimu iliyo bora sana” alisema Kasesela

Aidh Kasesela alisema kwanini kanisa la KKKT limekuwa kanisa ambalo limegawanyika katika kanda mbalimbali ambapo kila ukanda unafanya mambo bila kuwa na ushirikiano wowote ule na dayosisi nyingine.“Ukiangalia maisha ya viongozi wanaofanya kwenye kanda mbalimbali wanatofautiana kuanzia mishahara na maisha yao yamekuwa yanatofauti kubwa sana sasa nawaomba leo hii mliombee pia hili ili kanisa liwe na umoja” alisema Kasesela

Kasesela alisema kuwa mgawanyiko huo utasabisha vyou vingi vya KKKT kufa kutokana na kutokuwa na ushirikiano kama ilivyokuwa na vyuo vingine hapa.Kwa upande wake Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Iringa,Blaston Gavile aliwataka wanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa kukesha na kukiombea chuo hicho mara kwa mara.Ombeni nanyi mtapewa kwa kuwa mnaomna kwa nia njemba na mungu nimoto ambao unaweza kuwabariki kila mmoja wetu hapa hivyo nawaomba tena kuendelea kuomba” alisema Askofu Gavile

Askofu Gavile alimushukuru na kumpongeza mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela kwa utendaji wake wa kazi kwa wananchi wote kwa kuwa anaitendea haki nafasi hiyo anayoteuliwa na Rais.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...