Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MKUU wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar as Salaam Daniel Chongolo amezindua kampeni maalum ya kuhamasisha wananchi wa wilaya hiyo kulipa kwa wakat kodi ya majengo pamoja na kodi ya mabango.

Kampeni hiyo itakwenda sambamba na kampeni ya nyumba kwa nyumba kwa lengo la kuhakikisha wamiliki wote wa majenga wanalipa kodi kwa wakati na lengo la Wilaya ya Kinondoni ni kukusanya Sh.bilioni saba katika majengo.

Akizungumza na Michuzi Blog jijini Dar as Salaam wakati wa kuzindua kampeni hiyo kwa Wilaya ya Kinondoni iliyofanyika Bunju, Chongolo amesema lengo la kuzinduliwa kampeni hiyo ni kuhamasisha wananchi kuanza kulipa kodi ya majengo na mabango mapema.

Ameongeza kuna tabia ya wananchi wengi kujitokeza siku ya mwisho katika kulipa kodi ya majengo kiasi cha kusababisha msongamano mkubwa wa watu,hivyo Wilaya ya Kinondoni imeona ni vema ikaanza kampeni hiyo ili wananchi waanze kulipa kuanzia sasa  na mwisho ni Juni 30,2019.

Chongolo amesema katika kufanikisha kampeni hiyo viongozi wa ngazi mbalimbali wa Wilaya wakiwamo watendaji wa mitaa na kata watashirikiana na.maofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kwenda kufanya hamasa hiyo kwa wananchi na kubwa zaidi kutambua umuhimu wa kulipa kodi ya majengo na mabango.

"Kutakuwa na utaratibu maalumu wa kila mwenye jengo kupewa stakabadhi inayoonesha kodi anayostahili kulipa na kisha atakwenda kulipa na watendaji watakuwa wakiwaelekeza wananchi pakwenda kulipa kodi yao.

"Serikali kwa kuwajali wananchi wake imeamua kodi ya jengo kuwa moja tu iwe ni Sh.10,000 tu.Hivyo mwenye nyumba moja atalipa kiasi hicho na mwenye nyumba mbili atalipia kila nyumba kwa Sh. 10,0000.

"Kwa wenge ghorofa kila floo italipiwa sh.50,000.Makadirio yetu na matarajio ambayo tumejiwekea ni kukusanya Sh.bilioni saba kutoka kwenye majengo.Kampeni hii ambayo tumeizundua tunaomba wananchi washiriki kikamilifu ili kufikia malengo ambayo Wilaya ya Kinondoni tumejiwekea," amesema Chongolo.

Hata hivyo amesema baada ya kampeni ya kuhamasisha ulipaji wa kodi ya majengo,yeye mwenyewe kwa kushirikiana na viongozi wa Kara,mitaa na maofisa wa TRA watakwenda nyumba hadi nyumba kuangalia nani amelipa na na hajalipa kodi.Hivyo amesema cha msingi wananchi kulipa ndani ya muda uliowekwa.

 Kwa upande wake Meneja wa TRA Wilaya ya Kinondoni jijini Dar as Salaam Masawa Masatu amesema wamejipanga kuhakikisha kampeni hiyo inafanikiwa na watafanya hamasa maeneo yote ndani ya Wilaya huku akifafanua changamoto ya wananchi kusubiri tarehe za mwishoni wanataka kuiondoa.

"Kuna tabia ya baadhi ya wananchi ambao wao wanasubiri tarehe ya mwisho ndio wanakwenda kulipa kodi ya majengo.Kinondoni tunasema watu walipe kodi ndani ya muda uliopo kwani itaondoa msongamano kwenye maeneo ya kulipia kodi.Katika majengo tunakadiria kukusanya Sh.bilioni saba," amesema Masatu.

Wakati huo huo Mtendaji wa Kara ya Bunju Ibrahim Mabewa amesema kuwa jukumu lao ni kushiriki kikamilifu kuhakikisha hamasa ya wananchi kulipa kodi inafika kwenye.mitaa yote na hatimaye kodi ikusanywe kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania wote.

Naye Msanii maarufu nchini Mrisho Mpoto a.k.a Mjomba ambaye naye alishiriki kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo amesema wasanii wanalojukumu la kuhamasisha ulipaji wa kodi na kufafanua tena wanapaswa kuhamasisha kwa lugha rahisi ambayo itafanya mwananchi alipe kodi.

Amesema suala la kodi hata huko miaka ya nyuma inaelezwa namna lilivyokuwa ugumu maana unapozungumzia kodi unazungumzia fedha,hivyo kazi ya wasanii ni kutoa lugha rahisi lakini yenye kuzungumzia umuhimu ya wananchi kulipa kodi.
WASANII wa kundi la  ngoma za asili linaloongozwa na msanii nyota Mrisho Mpoto, wakitoa burudani kwa kutumia nyoka aina ya chatu, Barabara ya Bagamoyo eneo la Bunju A, ikiwa ni kuhamasisha wananchi kulipa kodi ya nyumba na mabango, wakati wa uzinduzi wa wiki ya ulipaji kodi hiyo, Wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, jana.(Picha na Christopher Lissa).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...