Na woinde Shizza globu ya jamii Arusha

Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro amefanya ziara ya kustukiza kukagua zoezi la utoaji wa vitambulisho vya wajasiliamali na wafanyabiashara ndogondogo katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Arumeru .

katika hali ya kuonesha kukerwa na kasi ndogo ya utoaji wa vitambulisho,Dc Murro  ilimlazimu kuvigawa vitambulisho hivyo yeye mwenyewe ,ziara hiyo ambayo aliifanya katika soko la Tengeru, kisha katika soko la usa River na hatimaye kumalizia katika soko la Ngaramtoni 

Muro amelazimika kwanza kutoa elimu kwa wafanyabiashara ndogondogo na wajasiriamali hatua ambayo iliongezeka mwitiko mzuri wa wafanyabiashara hao kuvichukua vitambulisho hivyo baada ya kuelimishwa na kuelewa umuhimu wa kuvitumia vitambulisho hivyo ambapo pia wananchi hao walimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kuwapatia vitambulisho 

Kwa upande Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa masoko ya Tengeru na USA River Abia Mbise amesema kuwa awali wafanyabiashara walikuwa na mwamko mdogo kutokana na kutopatikana kwa urahisi kwa vitambulisho hivyo.Aidha alipongeza kitendo cha mkuu wa wilaya kutoka ofisini na kuwafuata na kutoaelimu Wa umuhimu wa kuwa na vitambulisho hivi pamoja na kuvigawa yeye mwenyewe hatua hii imewasaidia kuongeza mwitiko kwa wafanyabiashara wengi kuchukua vitambulisho hivyo.

Akizungumza mara baada ya kutoa elimu na kugawa vitambulisho hivyo, alisema mkuu Wa Wilaya hiyo alisema ameamua kutoa vitambulisho hivyo Mara baada ya kuona zoezi hilo limezorota.

"nimelazimika kuingia mitaani kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wa utoaji wa vitambulisho hivi nimetoa maelekezo kwa wakurugenzi wa Halmashauri ya Meru na Arusha Dc pamoja na Maafisa Tarafa na watendaji wa kata na vijiji kuacha tabia ya kuwasubiria wafanyabiashara maofisini na badala yake watoke na kuwafuata ili kuwapunguzia usumbufu wa kwenda umbali mrefu kuchukua vitambulisho hivi" alisema Muro 
 Mkuu  wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro akieleza jambo wakati wa kugawa vitambulisho vya machinga katika solo la Tengeru
Picha malimbali zikionesha Mkuu  wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro akigawa vitambulisho vya machinga katika solo la Tengeru

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...