Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Dkt. Damas Daniel Ndumbaro(Mb.), amefanya mazungumzo na Balozi wa Italia nchini, Mheshimiwa Roberto Mengoni katika ofisi za wizara Dodoma. Katika mazungumzo hayo, miongoni mwa mambo mengine, Tanzania na Italia zimekubaliana kuendelea kushirikiana katika sekta za uwekezaji, utalii pamoja na kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia.
Mazungumzo yakiendelea.
Msaidizi wa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Charles Faini (wa kwanza na kulia) na Afisa wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Kisa Mwaseba (wa mwisho kushoto), wakifuatilia mazungumzo baina ya Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Daniel Ndumbaro(Mb.) na Balozi wa Italia nchini, Mhe Roberto Mengoni.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Daniel Ndumbaro (Mb.) na Balozi wa Italia nchini, Mhe Roberto Mengoni, wakiagana mara baada ya mazugumzo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...