Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.

Shirika la Railway Children limesema kuwa serikali imefanya mikakati mbalimbali yanayohusu watoto kilichobaki ni utekelezaji wa kwa halmashauri katika kuingiza mipango ya watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani lisiwepo.

Akizungumza na waandishi wa habari jiji Dar es Salaam Mkurugenzi Mkazi wa Shirika hilo Mussa Mugatta wakati akitangaza maadhimisho ya Siku ya Watoto wanaoishi na kufanya kazi mtaani ambayo hufanyika kila Aprili 12 ya mwaka, amesema ipo haja kwa mamlaka za serikali za mtaa kuingiza mipango ya watoto kutokana na serikali kuu imeweza kufanya kila kitu hivyo serikali za mitaa zinawajibu wa kugusa eneo watoto wanaoishi na kufanya kazi mtaani.

Amesema Railway Children inafanya kazi na majiji sita nchini katika kuhakikisha watoto wanaoishi na kufanya kazi mtaani linasimamiwa ili kuleta ustawi kwa watoto hao.

Mugatta amesema makundi yw watoto yapo 13 katika utekelezaji wa masuala ya watoto wanaoishi na kufanya kazi ni pamoja nchi kuridhia mkataba wa kimataifa wa umoja wa mataifa katika eneo la watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.

Aidha amesema kuwa watoto wanaoishi kazi wanatoka mkoa moja kwenda mwingine hivyo kwa Halmashauri lazima wafatilie kwa watoto wanaosafiri kujua wanakwenda wapi kwani baadhi wanatakiwa kuwa shule.

Mugatta amesema wananchi katika kukabiliana na watoto wanaoishi na kufanya kazi mtaani kila mmoja katika nafasi yaka anachukua hatua ya kuokoa kundi hilo.Amesema kama shirika linaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika juhudi za kuhakikisha watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani wanalindwa kutokuwepo.

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Railway Children Mussa Mugatta akizungumza na waandishi wa habari wakati akitangaza wiki ya maadhimisho Siku Watoto wanaoishi na kufanya kazi ambayo huadhimishwa kila Aprili 12 ya kila mwaka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...