Katika kuelekea sikukuu ya Pasaka, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limejipanga kikamilifu kuhakikisha wakazi wa Mkoa wa Mbeya, wageni na wakazi wa mikoa jirani wanasherehekea sikukuu hii kwa amani na utulivu. 

Kwa kutambua kuwa Mkoa wetu unapakana na nchi jirani ya Malawi pia barabara kuu inayounganisha nchi yetu na nchi jirani pamoja na mikoa jirani imepita hapa, tumejipanga vizuri kuhakikisha usalama kwa watumiaji wa barabara wakiwemo madereva na watembea kwa miguu. 

Wito wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya ni kwa watumiaji wote wa barabara kuzingatia sheria, alama na michoro ya usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.

Sambamba na hilo, tumejipanga vizuri kuhakikisha maeneo yeto tete kama vile Mlima Nyoka, Mlima Iwambi, Mlima Igawilo na Mwansekwa ulinzi na usalama umeimarishwa katika kipindi chote cha sikukuu ya Pasaka kama ilivyo kwa siku nyingine.

Kuelekea kipindi hiki cha sikukuu, waumini wa madhehebu ya Kikristu ushiriki katika ibada/misa kwa nyakati tofauti kulingana na ratiba zao, Jeshi la Polisi limejipanga kuhakikisha ulinzi na usalama katika makanisa hasa katika misa au ibada za mkesha. 

Aidha tunatoa wito kwa viongozi katika makanisa kuhakikisha wanaweka utaratibu mzuri hasa katika suala la ulinzi kwa kuzitumia kamati za ulinzi na usalama ili kuhakikisha ulinzi katika maeneo ya ndani na nje ya makanisa hasa sehemu za maegesho ya magari panakuwa salama kabisa.

Pia tunatoa rai kwa wamiliki wa kumbi za starehe kufuata sheria hasa kuzingatia leseni zao za biashara zinavyowaelekeza ikiwa ni pamoja na kuzingatia muda wa kufungua na kufunga sehemu zao za biashara, wenye kumbi za muziki kuhakikisha kumbi zao zinaingiza idadi ya watu inayohitajika [capacity] pamoja na kuweka walinzi katika maeneo yanayowazunguka.

Kuelekea msimu huu wa sikukuu ya Pasaka, ni wito wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa wazazi, walezi na jamii kwa ujumla kuzingatia ulinzi na usalama wa mtoto, pia kuwasaidia watoto kuwavusha katika maeneo tete kama vile barabara au maeneo yenye mito ili kuepuka madhara yanayoweza kuwapata. 

Pia ili kuepuka watoto kupotea katika kipindi hiki, wazazi na walezi wanapaswa kuongeza umakini, uangalizi kwa watoto wao kila mahali wanapokwenda iwe ni makanisani, misikitini au katika maeneo yenye michezo ya watoto.

Pia tunasitiza ulinzi na usalama katika makazi yetu, kuhakikisha kwa wale wanaotoka kwenda katika misa au ibada za mkesha kuacha waangalizi pia kuhakikisha tunajilinda kwa kufunga milango na madirisha ili kuepuka uhalifu katika nyumba zetu.

Aidha tunasisitiza utoaji wa taarifa za uhalifu na wahalifu kupitia namba za simu za viongozi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kama ifuatavyo:-
RPC…………………………………………………………….0715 009 931
RCO [Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa]………0658 376 052
STAFF OFFICER [Msaidizi wa RPC]………………….……0658 376 006
OPERATION OFFICER [Mkuu wa Operesheni Mkoa]..…..0754 466 924
RTO [Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa]……0658 376 472
OC FFU [Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia]……..…….0658 376 009
OCD MBEYA………………………………………………….0659 884 996
OCD MBALIZI………………………………………………..0655 248 381
OCD CHUNYA………………………………………………..0782 746 543
OCD MBARALI……………………………………………....0659 885 948
OCD RUNGWE……………………………………………….0659 885 253
OCD KYELA………………………………………………….0659 887 919

Imetolewa na:
[ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...