*Lazingira makazi ya Omar Al Bashir, Bint Alaa (22) azidi kuwa maarufu

Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii 

JESHI la Sudan linasubiriwa kutoa Kauli Muhimu mara  baada ya kuzingira makazi ya Omar Al Bashir ambaye amekuwepo madarakani kwa muda wa miaka 30.

Katika Maandamano ya kumlazimisha kiongozi huyo kung'oka madarakani, Binti Alaa Salah amekuwa ni Ishara ya Mapinduzi na amehusika katika kuchochea vijana kuingia mtaani kuidai 
Nchi Yao. Alaa ana miaka 22 na ni mwanafunzi wa uhandisi chuo kikuu cha kimaifa cha Sudan.

Maandamano hayo ya kumshinikiza Omar Al Bashir kung'oka madarakani yalianza Disemba mwaka jana na hiyo ni baada ya kupanda kwa gharama za maisha na bei ya mkate.

Ikumbukwe kuwa Kuna hati ya kumkamata Bashir iliyotolewa na Mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai (ICC.)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...