Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) imeotoa onyo kwa Kampuni za vyombo vya habari vya Sahara Media Group na African Media Group kutokana na kutangaza habari za magazeti baadhi ya habari kiundani.

Akizungumza wakati wa kutoa maamuzi ya kamati ya maudhui TCRA Mwenyekiti wa Kamati hiyo Vallerie Msoka amesema kuwa kituo cha Magic FM ilitangaza habari za habari magazeti katika kiundani ambayo ni kinyume na sheria ya zuio la Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt Harison Mwakyembe.

Amesema kuwa habari iliosomwa na Megic FM katika moja ya magazeti kuhusiana na matumizi ya kondomu ambapo watangazaji walikuwa wanadisi juu ya matumizi hayo.

Msoka amesema kuwa African Media Group katika utetezi wake walidai kuwa wakati linafanyika kosa hilo Megic FM ilikuwa chini ya umiliki mwingine na kuomba msamaha huo katika kamati hiyo.

Aidha amesema kuwa utetezi wa Megic FM haufanyi umiliki wa mtu mwingine kuharalisha utangazaji uliofanyika huku wakijua ni zuio la Waziri Habari, Utamaduni ,Sanaa na Michezo Dkt. Harison Mwakyembe Kwa upande wa Star Tv walitangaza habari ya Waziri wa Madini Dotto Biteko kiundani zaidi huku wakijua ni kosa kwa zuio la Waziri wa Habari,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Dk.Harison Mwakyembe.

Msoka amesema katika utetezi wake kampuni inayomiliki Star Tv ilisema kuwa wakati wanatangaza habari za magazeti aliyefanya hana uzoefu na kudai kuwa wale wazoefu wanaacha kazi.Amesema kuwa utetezi wa star tv haufanyi kuondoka kwa wafanyakazi ndio kutangaza habari za magazeti kiundani.
Amesema kuwa kwa vituo hivyo kama hawajalidhika wanaweza kukata rufaa ndani ya siku 21 pamoja kutaka kufuata sheria za utangazaji.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) Vallerie Msoka akitoa maazimio ya ukiukaji maudhui ya Utangazaji kwa Vituo vya Star Tv na Magic FM leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...