*Ni baada ya Kampuni hiyo kupata leseni ya kuonesha mashindano makubwa ya kukuza vipaji

*Amwambia Joseph Kusaga ubunifu, uthubutu wao ni fahari kubwa kwa nchi ya Tanzania

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

KAMPUNI ya Clouds Media Group wameandika tena historia! Hivyo ndivyo unavyoweza kuelezea baada ya kampuni hiyo kupewa leseni kamili ya kuendesha mashindano makubwa ya vipaji kwa Ukanda wa Africa Mashariki (East Africa’s Got Talent).

Mashindano hayo yatakuwa yanaonekana katika mabara mbalimbali na takribani nchi zaidi ya 58 duniani zitakuwa zikifuatilia hatua kwa hatua namna ya vipaji vinavyoibuliwa kupitia mashindano hayo.

Akizungumza Aprili 10 , 2019 katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk.Harrison Mwakyembe amesema anawapongeza Clouds Media Group kwa kufanikiwa kupata leseni ya kuonesha mashindano hayo makubwa kwani wameletea heshima nchi yetu ya Tanzania.

Dk.Mwakyembe amesema " Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Clouds Joseph Kusaga na Clouds Media kwa ujumla mnafanya kazi kubwa sana katika nchi yetu na mmeendelea kuwa mstari wa mbele katika ubunifu na kuthubutu .Kwa kitendo hiki cha kupata leseni ya kuonesha mashindano haya makubwa ya kukuza vipaji , tukiri mmetutoa tena kimaso maso na sina maneno ya kusema.Leo hii naweza kutamba na kesho nikiwa bungeni nitatamba sana.

"Hongereni sana Clouds Media Group na kama ambavyo Joseph Kusaga ameeleza mashindano haya yataangaliwa na mamilioni ya watu duniani, kwetu sisi kama nchi hii ni fursa kwetu ya kujitangaza, kama mnavyofahamu tuna vivutio vingi vya utalii lakini bado havijatangazwa vya kutosha lakini kupitia mashindano haya kwetu ni sehemu ya kujitangaza na tutaitumia vema,"amesema Dk.Mwakyembe.

Amefafanua kuwa kama kipindi kitaangaliwa na mamilioni ya watu duniani maana yake ni fursa kwa nchi kutumia show hiyo kujitangaza kadri inavyoweza na tayari Wizara yake imejipanga kutumia fursa hiyo.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group Joseph Kusaga wakati anazungumzia kupata leseni ya kuonesha mashindano hayo makubwa ya kukuza vipaji amesema kwa zaidi ya miaka 30 kampuni yao imejikita katika kutengeza fursa za kuhakikisha watanzania wenye vipaji wanapata nafasi ya kuonekana kufanikiwa kimaisha.

"Habari kubwa ya kiburudani ni kuzinduliwa rasmi kwa mashindano makubwa ya vipaji kwa ukanda wa Africa Mashariki (East Africa’s Got Talent). Mashindano haya yanaendeshwa kwenye mabara mbalimbali takribani nchi 58. Kwa mara ya kwanza katika historia Clouds Media Group tumepewa kamili (Franchised) ya kuendesha EAGT.

"Kwetu hili ni jambo kubwa na tunaamini tunakwenda kufungua fursa ya vijana wengi wenye vipaji mbalimbali, na kwa zaidi ya miaka 30 ya uwepo wetu tumekuwa tukiangalia namna ya kufungua fursa na maelfu ya vijana wa Tanzania wamefanikiwa,hivyo kama una kipaji chochote jiandae kwani tunakufungulia Dunia kuwa unachotaka,"amesema Kusaga.

Amefafanua zaidi pamoja na mambo mengine Clouds Media Group malengo yake ni kufungua milango kwa vijana wengi kwa kutengeneza Platfom ya kufungua fursa."Katika kuona hilo tuliona tunajaribu kila linalowezekana kufungua milango mingi zaidi na kubwa zaidi ni kupata International Brands na kisha kuzirudisha Tanzania ili kuinua vipaji vya vijana wetu."
Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe akizungumza mbele ya Wageni waalikwa (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa shindano hilo,Dkt Mwakyembe alisema "Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Clouds Joseph Kusaga na Clouds Media kwa ujumla mnafanya kazi kubwa sana katika nchi yetu na mmeendelea kuwa mstari wa mbele katika ubunifu na kuthubutu .Kwa kitendo hiki cha kupata leseni ya kuonesha mashindano haya makubwa ya kukuza vipaji , tukiri mmetutoa tena kimaso maso na sina maneno ya kusema.Leo hii naweza kutamba na kesho nikiwa bungeni nitatamba sana.

"Hongereni sana Clouds Media Group na kama ambavyo Joseph Kusaga ameeleza mashindano haya yataangaliwa na mamilioni ya watu duniani, kwetu sisi kama nchi hii ni fursa kwetu ya kujitangaza, kama mnavyofahamu tuna vivutio vingi vya utalii lakini bado havijatangazwa vya kutosha lakini kupitia mashindano haya kwetu ni sehemu ya kujitangaza na tutaitumia vema,"amesema Dk.Mwakyembe. PICHA ZOTE NA MICHUZI JR.
Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group Joseph Kusaga akifafanua jambo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi,Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe kuzindua rasmi shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar
Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group Joseph Kusaga akipiga makofi mara baada ya kumkaribisha mgeni rasmi,Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe kuzindua rasmi shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar
Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group Joseph Kusaga akipeana mkono na Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe mara baada ya kumkaribisha kuzungumza na Wageni waalikwa kabla ya uzinduzi wa shindano hilo

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe na Mkurugenzi wa Clouds Media Bw. Joseph Kusaga wakiwa na waratibu wengine wa tamasha hilo kutoka kushoto ni Mmoja wa waratibu Godfrey Mkama, Mchekeshaji kutoka Uganda Anne Kansiime na Lee Ndayisaba Mtayarishaji wa maudhui ya tamasha la , East Africa’s Got Talent.


Mkurugenzi Mkuu wa Cluds Medai Group Joseph Kusaga akiwa ameambatana na Mgeni rasmi Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk.Harrison Mwakyembe walipokuwa wakiwasili ukumbini kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar


Baadhi ya Wadau wakijadiliana jambo kabla ya uzinduzi rasmi wa shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar

Baadhi ya Wadau wakijadiliana jambo kabla ya uzinduzi rasmi wa shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar
Baadhi ya Wageni waalikwa wakiwa tayari kushuhudia uzinduzi rasmi wa shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar
Baadhi ya Wageni waalikwa wakijadiliana jambo kabla ya kushuhudia uzinduzi rasmi wa shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar
Mmoja wa Wadau akisubiri kushuhudia uzinduzi rasmi wa shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar
Baadhi ya Wageni waalikwa wakiwa tayari kushuhudia uzinduzi rasmi wa shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group Joseph Kusaga akifafanua jambo mbele ya wageni waalikwa kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi,Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe kuzindua rasmi shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar.

Baadhi ya Watangazaji Mahiri wa Clouds FM wakisubiri kushuhudia uzinduzi rasmi wa shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar



Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Fancy Nkuhi wa pili kutoka kushoto ni miongoni mwa wageni waliohudhuria katika hafla hiyo ya uzinduzi.
Muongozaji wa shughuli nzima (MC),ambaye pia ni mmoja wa Watangazaji mahiri wa Clouds FM,Masoud Kipanya akitoa muongozo wa namna ya shughili nzima ya uzinduzi eleza taratibu mbalimbali na ufafanuzi



Mchekeshaji maarufu kutoka nchini Uganda Anne Kansiime akifafanua jambo


Baadhi ya Wageni waalikwa wakiwa tayari kushuhudia uzinduzi rasmi wa shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar.

Baadhi ya Wageni waalikwa mbalimbali wakiwa tayari kushuhudia uzinduzi rasmi wa shindano la East Africa’s Got Talent,jijini Dar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...