Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

KANISA la Notre Dame lililopo Paris nchini Ufaransa likiwa ni  kanisa kubwa na mashuhuri duniani limeteketea kwa moto huku chanzo chako kikiwa hakijafahamika.

Polisi wamewataka raia kutokupita kwenye maeneo ya karibu ili kurahisisha uokoaji unaofanywa na vyombo vya usalama.

Meya wa Parid Anne Hidalgo ameeleza kuwa moto huo ni mkubwa na kuhakikisha kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vipo kazini katika kuzima moto huo.

Rais wa nchi hiyo Macron Emmanuel kupitia mtandao wa twitter ameeleza pia kusikitishwa na ajali hiyo huku akikanusha kuwa tukio hilo lilipangwa.

Kanisa hilo lililojengwa  kuanzia karne ya 13 na kukamilika karne ya 15 na huchukua watu zaidi ya million 13 kwa mwaka na hutembelewa na zaidi ya watu 30000 kwa siku.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...