Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
KANISA la Notre Dame lililopo Paris nchini Ufaransa likiwa ni kanisa kubwa na mashuhuri duniani limeteketea kwa moto huku chanzo chako kikiwa hakijafahamika.
Polisi wamewataka raia kutokupita kwenye maeneo ya karibu ili kurahisisha uokoaji unaofanywa na vyombo vya usalama.
Meya wa Parid Anne Hidalgo ameeleza kuwa moto huo ni mkubwa na kuhakikisha kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vipo kazini katika kuzima moto huo.
Rais wa nchi hiyo Macron Emmanuel kupitia mtandao wa twitter ameeleza pia kusikitishwa na ajali hiyo huku akikanusha kuwa tukio hilo lilipangwa.
Kanisa hilo lililojengwa kuanzia karne ya 13 na kukamilika karne ya 15 na huchukua watu zaidi ya million 13 kwa mwaka na hutembelewa na zaidi ya watu 30000 kwa siku.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...