Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa Mara nyingine tena imeshindwa kuanza kusikiliza kesi ya uchochezi inayowakibili viongozi tisa wa Chadema,  akiwemo Mwenyekiti wao Freeman Mbowe kutokana na kutokuwepo mshtakiwa Dk Vicent Mashinji  ambaye yuko Mkoani Ruvuma anahudhuria kesi ya uchochezi inayomkabili  mahakamani huko.

Mapema, wakili wa utetezi, Profesa Abdallah Safari aliwasilisha barua ya udhuru ya Dk Mashinji mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kusikilizwa ambapo katika barua hivyo, mshtakiwa ameomba ruhusa kuwa yuko Songea anakabiliwa kesi ya uchochezi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Songea.

Profesa Safari akisoma sehemu ya barua hiyo ameeleza kuwa kesi hiyo namba 9 ya mwaka 2017 imefika katika hatua ya utetezi na kwamba mshtakiwa Mashinji ameridhia kuendelea kwa usikilizwaji wa kesi inayomkabili katika Mahakama ya Kisutu.

Hata hivyo,  Wakili wa Serikali Mkuu Faraja Nchimbi amedai,  taarifa ya mshitakiwa haina vidhibitisho vya kutufanya sisi tukubaliane na hoja yao ya  kuendelea na kesi bila ya yeye kiwepo kwa sababu tangu tarehe ya mwisho ya kutajwa kesi hiyo ambayo inafika wiki mbili sasa mshtakiwa alikuwepo mahakamani . Tulitegemea mshtakiwa angeijuza Mahakama kuwa anakesi mahakama ya Songea.

Amedai ni vema mshtakiwa akatuambia kigezo gani ametumia asije kwenye mahakama hii na kwenda Songea

Aidha Wakili Nchimbi ameieleza  Mahakama kuwa, utaratibu wa kisheria  umeleelekeza kwenye sheria ya  mwenendo wa makosa ya jinai (CPA)  shauri lolote la jinai ikifika sehemu ya kuchukua ushahidi ni lazima ushahidi unapochukuliwa mahakami  uchukuliwe mbele mshtakiwa au washtakwa 

Amedai Licha ya  fungu la 197 (1b) sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai linatoa  mwanya kwa kutoa ushahidi isipokuwa mshitakiwa anapokuwa anamatatizo ya kiafya na awe anawakili pia awe ameridhia .

Amedai  suluhu pekee ni kuahirisha llshauri hilo na tarehe nyingine itakayopangwa mshtakiwa aje ajieleze kwa kina sababu za yeye kutofika mahakamani siku ya leo.

Kesi hiyo imeahirishwa  Mpaka kesho, Aprili 17.

Mbali ya Mbowe na Mashinji, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni,  Mbunge wa Iringa mjini, Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Taifa, Zanzibar, Salum Mwalimu,  Mbunge wa Kibamba, John Mnyika,  Katibu Mkuu Taifa, Vicent Mashinji,  Mbunge wa Kawe,  Halima Mdee,  John Heche na Mbunge wa Bunda,  Ester Bulaya.

Washitakiwa wanakabiliwa na mashitaka 13 likiwemo la kula njama, ambapo wote wanadaiwa kuwa, February 1 na 16, 2018, Dar es Salaam walikuĺa njama ya kutenda kosa la kufanya mkusanyiko usio halali na kukiuka tamko kutawanyika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...