Na woinde Shizza, Michuzi TV Arusha

Timu kitambi noma ya jijini Arusha imefanikiwa kuutwaa ubigwa na kuondoka na kombe Mara baada ya kuichapa timu ya Moshi veteran bao 1 kwao.

Hayo yote yalijiri Jana katika fainali ya bonanza la pasaka lililoandaliwa na timu ya kitambi noma ya jijini hapa ambapo katika bonanza hilo timu zaidi kumi imeshiriki zikimo za ndani ya nchi pamoja na nje ya nchi.

Timu ambazo zimeshiriki bonanza hill no pamoja na Moshi veteran ,mango garden veteran ya jijini dar es salaam, lushoto veteran ,Nairobi west ya Kenya ,Green Yard ya Kenya ,Sua Veterans ya Morogoro,Paris Fc Wa Nair obi, Makabe veterans pamoja na Arusha Coaches.

Akiongelea mashindano hayo Mwenyekiti Hamis Tembele alisema kuwa wameandaa mashindano haya kwa nia ya kukutanisha wadau na kubadilishana ,ujuzi ,biashara pamoja na undugu .

Alisema mashindano haya yanashindikisha Wazee ambao ni maveteran kutoka sehemu mbalimbali Wa ndani ya nchi pamoja na nje ya nchi.

Kwa upande wake msemaji Wa klabu ya kitambi noma ambaye ni waandaaji Wa bonanza hili LA pasaka Imma Diah alisema kuwa kwakuwa michezo ni furaha ajira na pia inatengeneza afya wameona waandae ili Wazee waendelee kujiburudisha na kuweka miili yao katika hali nzuri ya kiafya.

Kwa upande wake mthamini mkuu Wa mashindano haya Meneja masoko kanda ya kaskazini Wa kampuni Wa TBL Goodluck Kway ambao wamethamini bonanza hili kupitia kinyaji chao cha Konyagi alisema kuwa wameamua kuthamini bonanza hili kwakuwa linaamasisha michezo na wao kama wapo tayari kusaidia vitu vyote vinavyohamasisha amani na upendo.

Akiongea kwa niaba ya mkuu Wa mkoa Wa Arusha Mrisho Gambo,ambaye alikuwa mgeni rasmi Wa mashindano haya Afisa utamaduni Wa jiji LA Arusha Benson Maneno alisema aliwapongeza waandaaji Wa mashindano haya na kusema kuwa wamefanya jambo jema sana kuwakutanisha maveteran kutoka ndani ya nchi na nje ya nchi

Aliwasihi wasiishie pia kushabikia timu za verterani tu Bali waendelee at a katika timu zetu za mikoani pamoja na taifa.

Katika bonanza hili timu ya kitambi noma ilishika nafasi ya kwanza na kuondoka na kombe kubwa pamoja na zawadi ya box LA konyagi,mshindi Wa pili alikuwa ni Moshi veteran ambao wameondoka na kombe huku nafasi ya tatu imechukuliwa na timu ya Lushoto veteran ambao imeondoka na kombe Dogo.
Mdhamini Mkuu wa mashindano Meneja masoko kanda ya kaskazini Wa kampuni Wa TBL Goodluck Kway akimkabidhi zawadi mgeni rasmi Afisa utamaduni wa jiji la  Arusha Benson Maneno kwa kuwashukuru kuhudhuria katika bonanza hilo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...