Na Agness Francis blogu ya jamii. 

KAMPUNI ya kutoa mikopo ijulikanayo kama Kopa fasta imeamua kuunga mkono juhudi za wasanii wa sanaa za ufundi kwa kutoa fursa ya kutoa mikopo kwao ili kujiendeleza katika kazi zao za kisanaa zinazowapatia kipato hapa nchini. 

Akizungumza na vyombo vya habari leo Jijini Dar es Salaam Meneja wa Kopa Fasta Patrick Kang'ombe wakati wa uzinduzi wa mradi huo amesema kuwa kampuni hiyo inatoa mikopo kupitia makundi mbalimbali kwa wanachama ambao wamesajiliwa na wa miradi ya TACIP na PSGP inayotekelezwa na kampuni ya DataVision International kwa kushirikiana na taasisi na wizara za serikali. 

Kang'ombe amesema leongo la Kopa fasta ni kusaidia kuboresha sekta zisizo rasmi kama wasanii wa sanaa za ufundi ,ili kuwasaidikundia kuwa mikopo ya fedha na vitendea kazi, pamoja na kujenga uwezo kupitia mafunzo ya usimamizi wa fedha, biashara na uwekezaji. 

"Huduma yetu ni tofauti, kwani tumechagua sekta ambazo zimesahaulika na zimekuwa zikichukuliwa kuwa hazikopesheki, kwa maana ya kutokuwa na uwezo wa kuweka dhamana na kutoaminika kupewa mikopo, zimekuwa changamoto kubwa kwa sekta hizo, na kuzifanya kubaki nje ya mfumo rasmi pamoja na kuwa zimekuwa na mchango mkubwa katika pato la Taifa "amesema Kang'ombe. 

Aidha Meneja wa M-Lipa Maclean Geofrey ametoa ufafanuzi kuwa wanashirikiana na Kopa fasta katika mfumo ambao unawawezesha kupata malipo ambayo hayatumii fedha taslimu kukopa na kurejesha fedha. 

"Tunawawezesha makundi yasio rasmi kupata mkopo na kurejesha kupitia mfumo wa M-Lipa kupitia simu janja ya mkononi (Smartohone) pia msanii huyo wa sanaa za ufundi ili aweze kuomba na kupata mkopo anatakiwa awe mwanachama aliyesajiliwa na miradi inayofanya kazi na kopa fasta"amesema Maclean. 

Hata hivyo Mratibu wa ( TACIP) mradi wa utambuzi wa wasanii wa sanaa za ufundi Saul Mpock, amesema kuwa lengo la mradi huo ni kuwapa kipaumbele hapa nchini, kuwatengenezea mfumo wasanii hao ili waweze kukopesheka.
Meneja wa Kopafasta Patrick Kang'ombe pamoja na Wadau mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo wakikata keki kwa pamoja wakiashiria uzinduzi rasmi wa kopafasta leo Jijini Dar es Salaam.


Meneja wa Kopafasta Patrick Kang'ombe akifafanua lengo la kuwapa mikopo   wasanii wa sanaa za ufundi leo Jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa Kopafasta.
Baadhi ya wadau mbalimbali waliojitokeza katika hafla hiyo ya uzinduzi wa Kopafasta leo Jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...