Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani
Jafo pamoja na Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejeimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora, Mary Mwanjelwa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais
TAMISEMI, Mwita Waitara wakifuatilia michango ya wabunge wakati wa
kuchangia Bajeti ya Wizara TAMISEMI ya Mwaka wa Fedha 2019/2020 leo
Bungeni jijini Dodoma.
Mbunge wa kuteuliwa Mhe. Salma Kikwete akichangia hoja wakati wa
mjadala wa kuchangia Bajeti ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali
za Mitaa na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora leo Bungeni jijini Dodoma.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Mariam Kisiga
akichangia hoja wakati wa mjadala wa kuchangia Bajeti ya Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora leo Bungeni jijini Dodoma
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Subira Mgalu akiteta jambo na Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza
wakati wa kikao cha nane cha Mkutano wa 15 wa Bunge leo jijini Dodoma.
Baadhi ya wanafunzi kutoka Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA) kutoka
Tanga wakifuatilia shughuli za Bunge wakati wa kikao cha nane cha
Mkutano wa 15 wa Bunge leo jijini Dodoma.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe
akiteta jambo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Arise Amka Afika ya jijini
Arusha, Bi. Kuluthum Maabad alipomtembelea Bunge leo jijini Dodoma.
Taasisi ya Arise Amka Afrika inajishughulisha na masuala ya utoaji elimu
kuhusu harakati za ukombozi wa Bara la Afrika. (Picha na: Frank Shija -
MAELEZO)
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...