Na. Editha Edward

Kamishina msaidizi wa polisi mkoa wa Tabora ACP Emmanuel Nley kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya nzega wanawashikilia watu watano kwa uchunguzi zaidi kutokana na mauaji yaliyofanyika mapema hii leo katika kijiji cha Luzulo kata ya mizibaziba wilaya ya nzega mkoani Tabora .

Tukio la watu hao wamekamatwa na jeshi la polisi Baada ya mwanamke mmoja aliyefahamika kwa Jina la Nana Maganga (35) kujichukulia sheria mkononi ya kuwauwa watoto sita akiwemo mtoto mmoja wa kaka yake na watoto watano wa kuzaa mwenyewe 

watoto hao waliouawa ni pamoja na pala masanja (3) Shija Dotto(2) Nyawele Dotto (2) Sida Dotto (5) Kulwa Dotto (4) na Dotto Dotto (4)

Kwa upande wa mashuhuda wa Tukio hilo wameileza Michuzi Blog kuwa wamepokea taarifa za mauaji hayo kwa masikituko maana watoto hao walitegemewa kuwa viongozi wa taifa la kesho 

Aidha Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya nzega Bw. Godfrey Ngupula amewataka wananchi kutokujichukulia sheria mkononi za kutekeleza mauaji ya binadamu yeyote maana ni kinyume cha sheria na taratibu za Jamhuri ya muungano wa Tanzania na kuwataka wananchi kutoa taarifa katika vyombo vya sheria na vyanzo vya ulinzi na usalama kwa ajili ya kutafuta muafaka na njia sahihi.
Baadhi ya Wanakijiji wakiwa wamekusanyika kwa huzuni kwenye moja ya nyumba 

 Kamishina msaidizi wa polisi mkoa wa Tabora ACP Emmanuel Nley pamoja na Mkuu wa wilaya ya nzega Bw. Godfrey Ngupula  wakiwa katika eneo la tukio
 Kamishina msaidizi wa polisi mkoa wa Tabora ACP Emmanuel Nley pamoja na Mkuu wa wilaya ya nzega Bw. Godfrey Ngupula  wakiwa katika eneo la tukio 
 Moja ya kifaa kinachodaiwa kutumika kufanyia mauaji hayo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...