Na Agness Francis, Blogu ya Jamii. 

MSHAMBULIAJI wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC Mbaraka Yusuph anatarajia kukaa nje ya dimba kwa muda wa miezi tisa ijayo baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti jana jijini Cape Town huko nchini  Afrika kisini. 

Uongozi wa klabu hiyo umesema kuwa nyota huyo amekutwa na tatizo la kuchanika mtulinga wa kati wa goti lake la mguu wa kulia (Anterior Cruciate Ligament Tear), hali iliyomlazimu  afanyiwe upasuaji huo Katika Hospitali ya Vincent Pallotti iliyopo nchini Afrika kisini.

Yusuph amepata majeraha hayo wakati akiwa kwenye kikosi cha Namungo kinachoshiriki Ligi Daraja la Kwanza (FDL), iliyomchukua mchezaji hiyo kwa mkopo hadi mwisho wa msimu huu. 

Aidha Daktari wa Azam FC, Dr. Mwanandi Mwankemwa, aliyeongozana na mshambuliaji huyo nchini humo kushughulikia matibabu yake ametoa ripoti ya mchezaji huyo

Mwankema  amesema kuwa " Yusuph anatarajia kurejea tena dimbani kwa ajili ya ushindani Desemba 8 mwaka huu"

Kunako Ligi soka Tanzania bara Azam anatarajia kushuka dimbani April 14  mwaka huu wakiwa wageni dhidi ya Mbeya City Katika uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya majira ya Saa kumi jioni. 

Ambapo Katika mchezo uliopita kikosi cha Azam kilionekana kufanya vibaya  akilazimika sare ya bila kufungana dhidi ya Mbao FC  mechi iliyochezwa Jijini Mwanza CCM Kirumba. 

Wana lambalamba hao bado wanashikilia nafasi ya 2  kwa alama 63 wakiwa wameshacheza michezo 30 sawa na Yanga Sc mwenye alama 71 ambao ni Vinara wa  Ligi hiyo Tanzania bara, huku wekundu wa msimbazi Simba SC akiwa nafasi ya Tatu kwa pointi 57 ambaye Mpaka sasa anamichezo 22.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...