MENEJA wa Mamlaka ya Mapato  Tanzania (TRA) Wilaya ya Temeke Gamaliel Mafie anawakumbusha wafanyabiashara na wanunuzi kuendelea kujenga nidhamu ya kutoa risti na kudai risti pindi wanalifanya manunuzi. 

Amesema kuna adhabu kwa mtu ambaye hatoi na kudai risti na kimsingi adhabu yake ikibainika inafikia hadi shilingi milioni nne. na zaidi hivyo lazima mteja au mfanyabiashara atoe na kudai risti.

Mafie aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake Temeke Dar es Salaam ambapo alisema imekuwepo na changamoto hiyo ya watu kushindwa kudai risti pindi wanapofanya manunuzi.

Amefafua kuwa Mara nyingi wafanyabiashara na hata wateja hawana tabia ya kudai risti na kutoa hivyo basi TRA inawakumbusha kutekeleza sheria na kushindwa kufanya hivyo nikosa kama alivyotangulia kusema .

Amesema pindi mteja anapopewa risti au kutoa risti hiyo imeunganishwa kwenye mfumo wa ndani wa TRA ambayo inawezssha kujua kwamba ameuza au hajauza.

Akizungumzia Utoaji wa elimu alisema wao kama TRA wanajitahidi kutoa elimu kwa wafanyabiashara na hivi sasa wanajipanga kutoa elimu kwa kina kutokana na mabadiliko ambayo yamefanyika kupitia Bunge.

Amesema kwa asilimia 77 wanatoa elimu na wanaendelea kutoa elimu hiyo na kusisitiza kuwa ulipaji wa kodi ni lazima kwa kila mtanzania kulipa kodi ili mambo mengine katika nchi yaende.

Meneja Mafie alisema wanakuwa na mahusiano mazuri na walipa kodi japo wakati mwingine kunakuwa na hali ya kukimbizana nakwamba hiyo inatokana na baadhi ya wafanyabiashara kukwepa kulipa kodi.

" katika jambo hili ndugu waandishi hapa nishauri Serikali kuona namna ya kuazisha elimu kupitia elimu ya msingi ili.mwanafunzi anapoendelea kupata elimu basi ajuwe ipasavyo kuhusu kodi." Alisema Meneja

Mmoja wa maofisa wanaotoa elimu ya huduma kwa mlipa kodi Paul Magembe alisema wanafanya kazi hiyo kwa kuwatembelea vikundi mbalimbali ili kuwapa elimu ili kuona umuhimu wa kulipa kodi katika jambo ambalo wanalifanya.

Meneja wa TRA Temeke Gamaliel  Mafie

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...