Mhashamu Baba Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu katoliki Dodoma Beatus Kinyaiya amewataka Vijana kuwa mstari wa mbele kwenye kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii,kiuchumi na kisiasa ili kuijenga na kuistawisha Tanzania kwa kuwa ndio kundi kubwa linalotegemewa kwa kiasi kikubwa kwenye Kusukuma ajenda mbalimbali za kimaendeleo.

Baba Askofu Kinyaiya ameyasema hayo jana wakati wa adhimisho la Ibada ya Jumapili ya Matawi katika Kanisa la Mt. Yohana Mtume Kikuyu,Dodoma ambapo pia siku hii huwa ni maalum kwa ajili ya VIJANA WAKATOLIKI ULIMWENGUNI na kwa jana ilisimamiwa na VIJANA WAKATOLIKI WAFANYAKAZI*(VIWAWA)*

“Vijana wa Kanisa muwe mfano bora,ishini katika haki,upendo na kujituma na msiwe wasaliti wa nafsi zenu.Mfanye kazi kwa bidii na kujituma kwani Taifa linawategemea.Nimefurahi juu ya uanzishwaji wa Kituo cha Vijana ambacho kitatoa pia mafunzo ya Ufundi,jukumu la kukamilika kwake namuachia kijana mwenzenu Anthony Mavunde”-Alisisitiza Baba Askofu Mkuu Kinyaiya

Akizungumza katika Ibada hiyo,Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh Anthony Mavunde ,amewahidi Vijana hao kutoa ushirikiano wa kutosha katika kufanikisha ujenzi wa kituo hicho na akachangia Mifuko 100 ya saruji na fedha Tsh 1,000,000 na kuongoza harambee iliyopelekea kupatikana matofali 7000 ili ujenzi wa ukuta kuzunguka kituo uanze mara moja na pia kutoa ahadi ya kuwapatia vifaranga 500 kwa ajili ya mradi wa Kuku wa Mayai ili waweze kujiendesha kiuchumi.

“Baba Askofu Mkuu,mimi katika maisha yangu muda mrefu nilikuwa mtumishi wa Altareni kanisani na nimekuwa sehemu ya VIWAWA,namuomba Mungu atusaidie yote tuliyopanga leo yatimie ili kituo hichi kiwasaidie Vijana wengi hasa katika kutatua changamoto ya ukosefu wa Ajira”-Alisema Mavunde




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...