Na Ripota Wetu-Lagos, Nigeria

MKURUGENZI Mtendaji mpya wa Taasisi ya Tony Elumelu ya nchini Nigeria, Ifeyinwa Ugochukwu, ameanza majukumu yake mapya kuanzia Aprili 1, mwaka hu.

Ifeyinwa anakuwa Mkurugenzi Mtendaji wa tatu na wa kwanza kwa Afrika kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Tony Elumelu, ambapo kabla ya kuchukua nafasi hiyo aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Ushirikiano na Tahmini wa taasisi hiyo.

Desemba mwaka jana Taasisi ya Tony Elumelu ambayo inafanyakazi ya kuwawezesha wajasiriamali wa Kiafrika, ilitangaza uteuzi mpya wa Ifeyinwa kama Mkurugenzi Mtendaji nafasi ambayo ilikuwa ikishikiwa na mtangulizi wake Parminder Vir, ambaye kwa sasa anakwenda kuwa Mkurugenzi wa Bodi ya Ushauri wa Tony Elumelu.

Katika jukumu yake Ifeyinwa alisema atazingatia kuongeza umuhimu wa Programu ya Uwekezaji wa Tony Elumelu ya dola milioni 100 kwa kipindi cha miaka 10 na kuimarisha mahusiano kati ya Afrika na mfumo wa kimataifa wa ujasiriamali, kuwawezesha wajasiriamali wa Afrika na matokeo ya kujenga ajira na mali juu ya bara. 

Pia atachukua jukumu la kuweka nafasi ya TEF Connect- ambalo ni jukwaa la mitandao ya digital kwa wajasiriamali wa Afrika kama kitovu cha kuunda uhusiano wa biashara, kubadilishana uzoefu na kusambaza ujuzi kwa Bara la Afrika.

Katika kipindi cha miaka miwili Ifeyinwa Ugochukwu, alikuwa katika kutoa uzoefu wake hasa kupitia nafasi yakwe yake ya zamani ya Mkurugenzi wa Ushirikiano na Tathmini kabla ya kupata nafasi mpya ya kuongoza taasisi hiyo.

Taariga kwa umma iliyotolewa na Taasisi ya Tony Elumelu, ilieleza kwamba kwa nafasi yake mpya pia ni kiongozi anayethibitishwa na maono ya biashara kwa akili na uwezo wa kuwaleta watu pamoja. 

Ilielezwa kuwa uwezo wake wa namna ya kuisuka taasisi inavyostahili, kulingana na mazingira. Lakini pia ataangazia maendeleo na mazingira ya taasisi kwa kuona namna gani inaweza kupiga hatua zaidi.

Akizungumza kwa niaba ya Bodi ya Wadhamini, Tony Elumelu, Mwanzilishi wa Tony Elumelu Foundation alisema “Tuna hakika kwamba Ifeyinwa ndiye mtu makini wa kuimarisha Taasisi katika awamu yake ya uongozi. Uteuzi wake kama Mkurugenzi Mtendaji utaimarisha taasisi yetu ya kuongeza kiwango cha kujitolea na kufungua fursa katika mazingira ya ujasiriamali kote katika Bara la Afrika.

“Nimekuwa nikisema kuwa hakuna mtu wa ulitengeza Bara la Afrika, na maonyesho zaidi na utekelezaji wa azimio hili ni wajibu wetu wote,” alisema Mwasisi wa taasisi hiyo Tony Elumelu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...