Mvua iliyodaiwa kukwama Tanzania hatimaye imeanza kunyesha Kenya kwa kasi, huku wananchi wakiwa hawajajiandaa.

Wafanyabiashara waliokuwa wamepanga bidhaa zao pembezoni mwa barabara za jiji la Nairobi wameshindwa kufanya shughuli zao kutokana na mvua hizo.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la BBC, saa mbili kabla ya mvua hiyo kunyesha, idara ya hali ya hewa Kenya ilitangaza kuwa mvua itanyesha jijini Nairobi na maeneo mengine.

''Sikutarajia kwamba itanyesha na nilipokuwa nikiendelea na biashara yangu ilianza kunyesha  nikalazimika kutafuta hifadhi kwengineko,'' amesema mfanyabiashara mmoja nchini humo.

Wiki iliyopita naibu mkurugenzi wa idara hiyo, Bernad Chanzu alisema hakutakuwa na mvua msimu huu.

Wiki mbili zilizopita idara hiyo ilitangaza kuwa kiangazi kitaendelea mwisho wa mwezi huu huku mawingu ya mvua yakisalia Tanzania kutokana na kiwango cha chini cha upepo wa kusukuma mawingu hayo kuelekea Kaskazini mwa nchi hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...