Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle akimkaribisha Naibu Waziri Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Elias Kwandikwa kushoto alipowasili kufungua kikao cha baraza la wafanyakazi wa wakala huo kilichofanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la wafanyakazi wa wakala huo kilichofanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikua Naibu Waziri Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano  Elias Kwandikwa kushoto.
 Naibu Waziri Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Elias Kwandikwa akisoma hotuba wakati akifungua kikao cha Baraza la wafanyakazi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) kilichofanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
 Naibu Waziri Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano  Elias Kwandikwa (wa tatu kushoto) na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle (wa nne kulia) wakiimba wimbo maalumu wa wafanyakazi wa Mshikamano daima pamoja na viongozi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakati wa kikao cha Baraza la wafanyakazi wa wakala huo kilichofanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya mameneja wa mikoa wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wakisikiliza mada zilizokuwa zikitolewa wakati wa kikao cha Baraza la wafanyakazi wa wakala huo kilichofanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam ambacho kilihudhuriwa na Naibu Waziri Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Elias Kwandikwa.
Naibu Waziri Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Elias Kwandikwa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi waandamizi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) mara baada ya kumaliza kikao cha Baraza la wafanyakazi wa wakala huo kilichofanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO (TEMESA)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...