Afisa Mkuu Mkaguzi wa Ndani wa Benki ya NMB, Juma Kimori (kushoto) akimkabidhi msaada wa flana 250 Kamishna Msaaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP), Bertha Mende (kulia) kwa ajili ya wanamichezo wa Jeshi la Magereza Tanzania.


BENKI ya NMB imekabidhi msaada wa flana 250 kwa ajili ya wanamichezo wa Jeshi la Magereza Tanzania ambao wanaenda Zanzibar kushiriki kongamano la michezo. 

Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo, Afisa Mkuu Mkaguzi wa Ndani wa Benki ya NMB, Juma Kimori alisema ushirikiano mzuri wanaoupata kutoka kwa Jeshi la Magereza kibiashara kama wateja wao unawasukuma kushirikiana kila linapotokea jambo linaloitaji kushirikiana.

Aliwashukuru Jeshi la Magereza kwa kuwaamini na kuendelea kufanya kazi pamoja na kuwaomba kudumisha ushirikiano huo.

Kwa upande wake mwakilishi wa Jeshi la Magereza, akipokea msaada huo, Kamishna Msaaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP), Bertha Mende alisema wanafarijika kuona mara zote wanapoitaji ushirikiano na NMB wanawaunga mkono hivyo kuwahakikishia wataendelea kudumisha. Alisema NMB imekuwa ikiwasaindia mambo mengi bila kuchoka na kuwaomba waendeleze uhusiano huo.
Afisa Mkuu Mkaguzi wa Ndani wa Benki ya NMB, Juma Kimori akizungumza kabla ya kukabidhi msaada wa flana 250 kwa ajili ya wanamichezo wa Jeshi la Magereza Tanzania. Wa pili kulia ni Kamishna Msaaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP), Bertha Mende aliyepokea pamoja na Mrakibu Mwandamizi wa Magereza (SSP), M.A. Mlawa anayesimamia michezo katika Jeshi la Magereza akishuhudia (kulia). Kushoto ni Meneja Mwandamizi Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya NMB, Ally Ngingite.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP), Bertha Mende (katikati) akizungumza kuishukuru Benki yaa NMB kwa msaada wa flana ulizozitoa kwa wanamichezo wa Jeshi la Magereza nchini. Kushoto ni Afisa Mkuu Mkaguzi wa Ndani wa Benki ya NMB, Juma Kimori pamoja na Mrakibu Mwandamizi wa Magereza (SSP), M.A. Mlawa anayesimamia michezo katika Jeshi la Magereza (kulia).
Picha ya pamoja mara baada ya hafla ya makabidhiano kwa pande zote mbili.
Baadhi ya wageni waalikwa na wafanyakazi wa NMB wakishuhudia tukio hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...