Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
Wakala wa Afya wa Usalama Mahala Pa Kazi (OSHA) imesema kuwa OSHA imekuwa sehemu ya watu wengine kujifunza kutokana na utoaji wa huduma sehemu za kazi.

Akizungumza na waandishi habari Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa OSHA Joshua Matiko  wakati wa ugeni wa Wizara ya Kazi ,Uwezeshaji ,Wazee,Wanawake na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar walipotembelea  OSHA kwa ajili ya kujifunza utoaji wa usalama wa afya mahala Pa Kazi.
Matiko amesema kuwa nia ya OSHA ni kuwa Taasisi kubwa ya watu kujifunza masuala ya utendaji mahala pakazi na kuweza kupata tija.

Amesema kuwa serikali ya mapinduzi kuja kujifunza licha ya kubadilishana mawazo inaunganisha udugu uliopo kati ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani. Matiko amesema kuwa Zanzibar kwenda kujifunza sio peke yao bali hadi taasisi za nje zimefika kujifunza na kwenda kwao kuunda chombo kama OSHA.Kaimu Mkurugenzi Mkuu huyo amesema kutokana na kutoa elimu kwa ajili kumepungua kwa magonjwa na majanga mahala pakazi kutokana na elimu wanayoitoa.

Nae Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee ,Wanawake na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Shadia Mohamed Suleiman amesema kuwa OSHA wana vitu vizuri ambapo tukienda  kufanyia kazi tutaweza kupata mabadiliko katika mahala pakazi. Shadia amesema kuwa licha ya kujifunza ni pamoja na kuishauri serikali kuanzisha wakala inayojitegemea ili iweze kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maendeleo, Wanawake ,Habari ,Utalii na Vijana Mwantatu Mbaraka Khamis amesema OSHA imezatiti katika kulinda usalama wa afya mahala pakazi kutokana na utendaji wake pamoja na kuwa  wataalam wenye uwezo wa kufanya kazi hiyo.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Afya wa Usalama Mahala Pakazi (OSHA) Joshua Matiko akizungumza kuhusiana na ugeni kutoka Zanzibar kujifunza katika wakala huyo.
 Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji,Wazee ,Wanawake na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Shadia Mohamed Suleiman akizungumza kuhusiana na ujio wao katika Wakala wa Afya wa Usalama Pahala Pakazi (OSHA) jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji,Wazee ,Wanawake na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Shadia Mohamed Suleiman akiwa katika picha ya pamoja na kamati ya Bunge na Kaimu Mkurugenzi OSHA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...