Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.), leo tarehe 9 Aprili, 2019 akiwa jijini Dodoma amefungua rasmi Kongamano la kwanza la Uwekezaji pamoja na Mkutano wa mwaka wa Diaspora wa Tanzania linalofanyika nchini Sweden. Ufunguzi wa kongamano hilo ulirushwa moja kwa moja na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1). Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Kasidi Faraji Mnyepe, wakifuatilia kongamano hilo lililorushwa moja kwa moja na TBC 1 huku wao wakiwa Dodoma.
Kongamano likiendelea.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...