Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
MKUU  wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda leo April 10 ametimiza ahadi yake aliyoitoa  ya kuwapatia wajane kiasi cha Shillingi milioni 10 za kusaidia kutatua changamoto za kiofisi zilizokuwa zikiwasumbua wajane na hiyo ni pamoja na malimbikizo ya madeni ya kodi kwenye nyumba wanayoitumia kama ofisi.

Inakumbukwa kuwa Aprili 4 wakati wa kongamano la wajane Makonda alitoa ahadi ya kuwapatia wajane hao kiasi cha shilingi milioni 10 na kuwatafutia eneo la kujenga jengo la ofisi za makao makuu ya chama cha wajane nchini na tayari eneo hilo limepatikana tayari kwa kuanza ujenzi.

Mapema leo Afisa elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam Hamis Lissu amewakabidhi wajane hoa kiasi cha shilingi milioni 10 kwa niaba ya RC Makonda ambaye yupo katika majukumu mengine ya kitaifa.

Kwa upande wao wajane hao wamemshukuru RC Makonda kwa kuwasaidia kutatua changamoto mbalimbali zilizokuwa zikiwakabili na wanaamini kupitia uongozi thabiti wa RC huyo ujenzi wa jengo la makao makuu ya chama hicho utakamilika kwa uharaka.
 Afisa elimu na katibu tawala msaidizi wa Mkoa wa Dar es Salaam Hamis Lissu (kulia) akikabidhi fedha takribani ya shilingi milioni 10 kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Paul Makonda kwa mwenyekiti wa wajane Rose Sarwatt leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti na Mkurugenzi wa chama cha wajane nchini Rose Sarwatt akionesha fedha walizopewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Mokonda kwa ajili ya uendeshaji wa ofisi, leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...