NA MWAMVUA MWINYI, PWANI

JESHI la polisi mkoani Pwani, limepiga marufuku kupiga disko toto pamoja na kuwaasa wamiliki wa kumbi za starehe kuacha kujaza watu wengi kuzidi uwezo wa kumbi zao, kwenye sikukuu ya pasaka.

Aidha limejipanga kufanya msako na doria ili kuhakikisha hakuna tukio la kihalifu litakalofanikiwa kuelekea sikukuu hiyo.

Kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP) Wankyo Nyigesa aliwatahadharisha, wamiliki hao kuzingatia sheria na atakaekiuka agizo hilo hatua zitachukuliwa dhidi yao.

Katika hatua nyingine ,aliwataka watumiaji wa vyombo vya moto kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuzuia ajali katika barabara za mkoa huo.

Wankyo alisema, madereva wasiendeshe baada ya kutumia vileo kwani askari wao wa kikosi cha usalama barabarani wapo kila kona hivyo hawatoweza kupita mkoani humo,pasipo kukaguliwa .

"Kwa wamiliki wa magari yanayosafirisha abiria kuzingatia uwepo wa madereva wawili na magari yatakayobainika kuwa na dereva mmoja hayataruhusiwa kuendelea na safari"

Kamanda huyo hakusita kuwaomba wazazi na walezi kuweka ulinzi majumbani mwao endapo watatoka kwenda kwenye nyumba za ibada na kuwawekea waangalizi watoto watakapowaacha nyumbani.

WAKATI HUO HUO, jeshi hilo linamshikilia Mwamini Shomary (37) ,mkazi wa Yombo Bagamoyo kwa kosa la kusafirisha mafuta ya kula dumu kumi yenye thamani ya laki tano, ambayo hayajalipiwa ushuru.

"Askari wetu wakiwa doria maeneo ya Kwamatias, huko Kibaha walimkamata mtuhumiwa akiwa na mafuta hayo aina ya mico gold ujazo wa lita 20 kila moja akitokanayo Bagamoyo.

Wankyo alielezea kwamba, mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Kamanda huyo aliongeza kusema, pia wamekamata bangi puli tano, kete 155 na pombe aina ya gongo lita 11.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...