Na Karama Kenyunko,Globu ya jamii

WAZIRI wa  Nchi,Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira),Januari Makamba amesema kwamba katazo la kuzuia matumizi ya mifuko ya plastiki nchini litakuwa la kisheria na kanuni zake zitakazokuwa na adhabu kwa wale watakaokiuka.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Makamba pia amesema katika kipindi hichi cha mpito,wizara yake itaweka utaratibu wa mahali pa kuiweka,sehemu ya kuisalimisha na kuiteketeza kwa walio na mifuko hiyo katika magodauni yao kabla haijawa kosa kisheria kwa muda uliowekwa na Serikali.

Kwa kukumbusha tu,mapema wiki iliyopita Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa bungeni Mjini Dododma,alisema kuanzia Juni Mosi mwaka huu, itakuwa ni marufuku kutengeneza, kuuza, kuingiza na kutumia mifuko ya plastiki kwa ajili ya kubebea bidhaa za aina yoyote.

Hivyo Waziri Makamba wakati anazungumza na wadau wa mifuko ya plasiki, kuhusu fursa za uwekezaji katika uzalishaji wa mifuko mbadala ya plastiki amefafanua katazo hilo litakuwa la kisheria na sio tamko.

Ameongeza kuwa katazo hilo  ni kuanzia uzalishaji, kuuza, kuingiza, kumiliki, kuhifadhi kutumia,yote hayo ni makosa.Kanuni hizo watakazoweka zitakuwa na adhabu kwa watakaokiuka hata atakayekutwa naye na kutakuwa na faini au vifungo kwa mujibu wa sheria,kanuni zitakapokamilika zitatangazwa"alisema Makamba

Pia amesema katazo hilo halitausisha vifungashio vya plastiki kwa bidhaa kama Korosho,maziwa, na nyinginezo bali litaanza kwa mifuko ya plastiki inayotumika kubebea bidhaa.

Wakati huo huo Makamba amesema uwamuzi wa katazo hilo si wa gafla kama inavyosemwa na baadhi ya wamiliki wa viwanda vya kutengeneza mifuko ya plastiki kwani inafahamika tangu Agosti mwaka 2016 kwa wadau kuandikiwa barua kujadili  kupiga marufuku mifuko hiyo.

Makamba amesema katazo hilo lina manufaa kwa taifa kàtika kutunza mazingira na kwamba kwa mwaka mifuko bilioni 3 inaishia katika fukwe za mito,bahari na kukaa muda mrefu ikichafua mazingira.
  
Kwaupande wake ,Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Joseph Kakunda amewataka watakaopewa mamlaka ya kusimakia katazo hilo kutolichukulia kama fursa ya kuomba na kupokea rushwa.

Kwa baadhi ya mawakala na wafanyabiashara wa mifuko ya plastiki kutoka Sokoni Kariakoo wameiomba serikali iwaongezee muda wa kuiuza hadi Januari mwakani, kwani bado ipo mingi na wanadaiwa na wafanyabiashara raia wa china waliowapa.

Hat hivyo,Waziri Mahakama akijibu hoja hiyo,alisisistiza kuwa katazo hilo ni msimamo  wa Serikali na halitarudi nyuma hivyo wakae na waliowauzia kuona kama watawalipa fidia ama la.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...