Na Grace
Semfuko-MELEZO
Serikali inaandaa
Mpango Maalum wa kuimarisha na kuongeza wawekezaji katika sekta mbalimbali
ikiwepo ya mifugo na Kilimo ili kuongeza upatikanaji wa nyama,siagi na Maziwa
pamoja na Chakula nchini.
Waziri wa Nchi Ofisi
ya Waziri Mkuu anaeshughulikia Uwekezaji Angela Kairuki amesema Mpango huo
unaanza na kuzungumza na wawekezaji katika nchi mbali mbali duniani ambao wana
uwakilishi wa kibalozi nchini Tanzania.
Kairuki aliyasema
hayo ofisini kwake jijini Dar Es Salaam mara baada ya kufanya mazungumzo na
mabalozi watatu wanaoziwakilisha nchi zao akiwepo Balozi wa Afrika Kusini
Bw.Thamsanqa Dennis Mseleku, Balozi wa Ilerand Be.Paul Sharlock na Balozi wa
Marekani nchini Tanzania Bi Imni Paterson ambao kwa nyakati tofauti wamemweleza
Waziri kuwa wamekuwa na Mpango madhubuti wa kuongeza wawekezaji Binafsi ili
kuinua uchumi na kuongeza ufanisi wa bidhaa za viwanda.
Kairuki alisema
Serikali inaandaa mikutano mikubwa na wawekezaji wa nchi hizo Jijini Dar Es
Salaam ambapo ataanza na wawekezaji wa China utakaofanyika April 17 mwaka huu
ukihusisha pia taasisi mbali mbali za Serikali zinazosaidia uwekezaji ili
kuangalia fursa,kushauriana na kusikiliza changamoto za Uwekezaji nchini.
Kwa upande wake
Balozi wa Ireland nchini Tanzania Bw. Paul Sharlok alisema nchi yake inaendelea
kuhamasisha wawekezaji na kutangaza vivutio vyilivyopo Tanzania ambapo katika
mkutano Mkubwa wa Kiuchumi wa Ireland na Afrika
unaofanyika mara moja kwa miaka miwili kwa mwaka jana walipendekeza
kuwekeza kwenye sekta ya kilimo Biashara na kuwaunganisha wawekezaji wa Ireland
na Tanzania katika kufanya kazi pamoja.
"Sisi Ireland
tuna Mpango maalum kuhusu uchumi wa Afrika, kila baada ya miaka miwili tunakuwa
na mkutano Mkubwa wa kiuchumi wa Ireland na Afrika, mwaka Jana tulizungumzia
Kilimo Biashara na tuliweza kuwaunganisha wafanyabiashara wengi wa Tanzania,
mwakani tutafanya mkutano huo natumaini sekta Binafsi na Kituo cha Uwekezaji
Tanzania TIC watashiriki" alisema Balozi sharlock.
Nae Balozi wa
Marekani nchini Tanzania Imni Paterson alisema kwa muda mrefu Marekani imekuwa
na mikakati mingi ya kiuchumi kuhusu Tanzania, wataiendeleza mikakati hiyo na
pia wataanzaa mkutano wa pamoja baina ya Wizara ya Uwekezaji na wawekezaji wa
kimarekani ili kupata majadiliano ambayo yatasaidia pande zote.
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, Angellah Kairuki akifafanua jambo kuhusu sekta ya uwekezaji nchini kwa Balozi wa Ufaransa Nchini Tanzania, Frederic Clavier alipomtembelea leo Ofisini Kwakwe Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Angellah Kairuki akifafanua jambo kuhusu sekta ya uwekezaji nchini kwa Balozi wa Norway nchini, Elisabath Jacobsen walipokuatana leo Ofisini Kwakwe Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Angellah Kairuki akifafanua jambo kuhusu sekta ya uwekezaji nchini kwa Balozi wa Norway nchini, Elisabath Jacobsen walipokuatana leo Ofisini Kwakwe Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, Angellah Kairuki, akifafanua jambo kwa Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo kutoka Marekani USAID, Andy Karas katika mazungumzo mafupi yalifanyika Ofisini Kwakwe Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, Angellah Kairuki akizungumza na Balozi wa Uholanzi nchini, Jeroen Verheul, alipomtembelea Ofisini Kwakwe Jijini Dar es Salaam. (Picha na Paschal Dotto-MAELEZO)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...