Na Grace Semfuko-MELEZO

Serikali inaandaa Mpango Maalum wa kuimarisha na kuongeza wawekezaji katika sekta mbalimbali ikiwepo ya mifugo na Kilimo ili kuongeza upatikanaji wa nyama,siagi na Maziwa pamoja na Chakula nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia Uwekezaji Angela Kairuki amesema Mpango huo unaanza na kuzungumza na wawekezaji katika nchi mbali mbali duniani ambao wana uwakilishi wa kibalozi nchini Tanzania.

Kairuki aliyasema hayo ofisini kwake jijini Dar Es Salaam mara baada ya kufanya mazungumzo na mabalozi watatu wanaoziwakilisha nchi zao akiwepo Balozi wa Afrika Kusini Bw.Thamsanqa Dennis Mseleku, Balozi wa Ilerand Be.Paul Sharlock na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Bi Imni Paterson ambao kwa nyakati tofauti wamemweleza Waziri kuwa wamekuwa na Mpango madhubuti wa kuongeza wawekezaji Binafsi ili kuinua uchumi na kuongeza ufanisi wa bidhaa za viwanda.

Kairuki alisema Serikali inaandaa mikutano mikubwa na wawekezaji wa nchi hizo Jijini Dar Es Salaam ambapo ataanza na wawekezaji wa China utakaofanyika April 17 mwaka huu ukihusisha pia taasisi mbali mbali za Serikali zinazosaidia uwekezaji ili kuangalia fursa,kushauriana na kusikiliza changamoto za Uwekezaji nchini.

Kwa upande wake Balozi wa Ireland nchini Tanzania Bw. Paul Sharlok alisema nchi yake inaendelea kuhamasisha wawekezaji na kutangaza vivutio vyilivyopo Tanzania ambapo katika mkutano Mkubwa wa Kiuchumi wa Ireland na Afrika  unaofanyika mara moja kwa miaka miwili kwa mwaka jana walipendekeza kuwekeza kwenye sekta ya kilimo Biashara na kuwaunganisha wawekezaji wa Ireland na Tanzania katika kufanya kazi pamoja.

"Sisi Ireland tuna Mpango maalum kuhusu uchumi wa Afrika, kila baada ya miaka miwili tunakuwa na mkutano Mkubwa wa kiuchumi wa Ireland na Afrika, mwaka Jana tulizungumzia Kilimo Biashara na tuliweza kuwaunganisha wafanyabiashara wengi wa Tanzania, mwakani tutafanya mkutano huo natumaini sekta Binafsi na Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC watashiriki" alisema Balozi sharlock.

Nae Balozi wa Marekani nchini Tanzania Imni Paterson alisema kwa muda mrefu Marekani imekuwa na mikakati mingi ya kiuchumi kuhusu Tanzania, wataiendeleza mikakati hiyo na pia wataanzaa mkutano wa pamoja baina ya Wizara ya Uwekezaji na wawekezaji wa kimarekani ili kupata majadiliano ambayo yatasaidia pande zote.
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, Angellah Kairuki akifafanua jambo kuhusu sekta ya uwekezaji nchini kwa Balozi wa Ufaransa Nchini Tanzania, Frederic Clavier alipomtembelea leo Ofisini Kwakwe Jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Angellah Kairuki akifafanua jambo kuhusu sekta ya uwekezaji nchini kwa Balozi wa Norway nchini, Elisabath Jacobsen walipokuatana leo Ofisini Kwakwe Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Angellah Kairuki akifafanua jambo kuhusu sekta ya uwekezaji nchini kwa Balozi wa Norway nchini, Elisabath Jacobsen walipokuatana leo Ofisini Kwakwe Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, Angellah Kairuki, akifafanua jambo kwa Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo kutoka Marekani USAID, Andy Karas katika mazungumzo mafupi yalifanyika Ofisini Kwakwe Jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, Angellah Kairuki akizungumza na Balozi wa Uholanzi nchini, Jeroen Verheul, alipomtembelea Ofisini Kwakwe Jijini Dar es Salaam. (Picha na Paschal Dotto-MAELEZO)


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...