Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Mh. Harusi Suleiman amezitaka Hospitali ya
Taifa Muhimbili-MNH- na Mnazi Mmoja kudumisha uhusiano na ushirikiano
uliopo ili kuwaenzi waasisi wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Naibu Waziri Suleiman ametoa kauli hiyo katika hafla ya kuhitimisha tamasha la
Pasaka 2019 lililofanyika Visiwani Zanzibar na kuhusisha timu za michezo za
Muhimbili pamoja na Hospitali ya Mnazi Mmoja iliyopo visiwani humo.
Akizungumza katika hafla hiyo amesisitiza kwamba timu hizo zimekuwa
zikikutaka kila mwaka kwa lengo la kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya pande
hizo mbili ambapo mwaka jana tamasha hilo lilifanyika Tanzania Bara.
“Ndugu zangu tumefarijika kuja kututembelea katika pasaka hii tunaomba
ushirikiano huu uendelezwe kwa faida ya pande zote mbili, pia kikubwa
nilichofurahishwa kutoka kwenu ni nidhamu pamoja na maadili kwani hata katika
michezo tunasisitiza nidhamu na maadili hakika mnastahili pongezi”. Amesema
Naibu Waziri wa Afya Zanzibar.
“Lakini pia yapaswa kuwashukuru viongozi wetu ambao walianzisha muungano
wetu ambao umetuwezesha kushirikiana katika nyanja mbalimbali ikiwemo
michezo hivyo hatuna budi kuwaenzi kwa kuendeleza na kuiboresha zaidi michezo
hii ambayo ilianzishwa mwaka 1972”. Amesisitiza Mh. Suleiman.
Kwa upande wa Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi kutoka Muhimbili
Dkt. Praxeda Ogweyo, amewapongeza wanamichezo wote walioshiriki katika
tamasha la Pasaka 2019 na kueleza kuwa Hospitali ya Taifa Muhimbili ipo mstari
wa mbele katika kuhakikisha michezo inaendelezwa katika taasisi hiyo na kutoa
fursa kwa watumishi wengi kushiriki.
Naibu Waziri wa Afya Mh. Harusi Suleiman akizungumza na wanamichezo katika hafla ya ufungaji wa tamasha la pasaka liliofanyika Zanzibar na kuhusisha timu za Hospitali ya Taifa Muhimbili na Hospitali ya Mnazi Mmoja.
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi Dkt. Praxeda Ogweyo, akitoa neno la shukrani wakati wa kufunga tamasha hilo.
Baadhi ya wanamichezo wakikiliza neno kutoka kwa Naibu waziri wa Afya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...